Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa jina naitwa Edwin Sannda, wengi huwa wakisikia hili jina wanashtuka kidogo; lakini msishtuke, Sannda hii ni nzuri tu, siyo kama ile ya kuzikia. Ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Mjini. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, nachukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuwepo hapa, lakini pia nikishukuru chama changu kwa kupitisha jina hatimaye likaenda kupigiwa kura. Nawashukuru wadau wangu wote, familia, ndugu jamaa na marafiki na hatimaye wapiga kura wa Jimbo la Kondoa Mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, moja kwa moja napenda kuchangia kwenye hotuba ya Rais. Kwanza kabisa naipongeza; imekaa vizuri, imegusa nyanja zote, lakini pia nawapongeza kwa wale waliotupa Mpango wa miaka mitano wa Maendeleo, wameakisi moja kwa moja hotuba ya Rais, wamegusa kila nyanja, nawapongeza sana. Pia yule aliyewasilisha ule mpango ni pacha wangu, kwa hiyo naye nampongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nichangie pale kwa maana ya vitu vikubwa vinne. Mpango mzuri, lakini huwa tatizo letu linakwenda kwenye utekelezaji (execution). Nawaomba hasa wale Wizara ya Fedha na Mipango na Serikali nzima kwa ujumla, suala la utekelezaji ndiyo liwe msingi mkubwa wa kuangalia (execution). (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, yameongelewa mengi sana kuhusiana na government efficiency na effectiveness (ufanisi wa Serikali), lakini kila tunapoongelea ufanisi wa Serikali, tunazungumzia kupunguza gharama na kubana matumizi. Napenda pale kwenye suala la efficiency ya Serikali tuongezee suala la delivery time, kukamilisha miradi, kufikisha huduma na yenyewe mwisho wa siku inaingia kwenye gharama. Tukiweza kufanikisha eneo hili napo tutakuwa tumefanya vizuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mbali na delivery pia suala la ubora. Tunatengeneza vitu, tunakamilisha miradi chini ya viwango, hatimaye tunahitaji kufanya marekebisho muda siyo mrefu, ambayo pia ni gharama tena.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwenye government efficiency, labda tungeangalia sehemu tatu, gharama inavyozungumziwa ya kwanza, delivery time, pamoja na quality ya huduma zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu cha tatu ningependa kuzungumzia suala la ubunifu kidogo. Kila mmoja aliyesimama kati yetu hapa anavutia kwake, tatizo liko hili, huduma zinahitajika hizi lakini mwisho wa siku ni lazima tujue ni namna gani tutatoka nje ya box tuwe wabunifu kuongeza kipato chetu. Tukiwa na kipato kikubwa kabisa kama nchi, ina maana hizi huduma zote zitafika, siyo tunagombea zile rasilimali chache. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nafikiri, tujaribu kuangalia kama inawezekana, maana na sisi wenyewe ndio tunaotunga sheria, tukawekeza kwenye baadhi ya sekta. Hawa wawekezaji wakubwa wanaokuja au sekta ambazo tutaziona ni nzuri kabisa zitatuletea tija, mbali na kodi tunayopata, vyanzo vya kawaida vya mapato ya Serikali, lakini tuwe na hisa tuwekeze ili tuwe tunapata magawio yaongeze katika Pato zima la Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri Wizara ya Fedha pamoja na nyingine, hebu tuangalie eneo hili, kama litahitaji sheria ya kubadilishwa au kutungwa, siyo kwamba tunaenda kufanya biashara per se lakini angalau tuwe na uwekezaji na sisi tuongeze vyanzo vya mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho ninalotaka kuongea ni suala la…
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.