Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kitu kinaitwa the wind of change au kwa tafsiri yangu mwenyewe, upepo wa mabadiliko. Huko nyuma waliosoma zamani ilikuwa ukichaguliwa kwenda Shule ya Serikali unaona wewe ndio umefanya vizuri na watu hawakuwa tayari kwenda private schools, hilo ni jambo lilikuwa huko nyuma. Wote waliobahatika kwenda Shule za Serikali, walionekana wamefanya vizuri na wenzetu wachache walioenda shule za private walionekana kana kwamba hawakufanya vizuri. Liliendelea hilo kwa muda wote na watu waliziheshimu Shule za Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa muda huu tujiulize, tumekosea wapi? Tujiulize tu swali hilo la msingi, tumekosea wapi? Tukishapata majibu, tutajua. Hata hii habari kwamba kuwe na ada elekezi au zisiwepo, ni suala tu la kujiuliza, tumekosea wapi ikiwa huko nyuma watu walipenda Shule za Serikali? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini katika haya yafutayo: kwa kuuliza wewe ni mjinga kwa dakika chache, kwa kutouliza, wewe unakuwa ni mjinga milele. Kwa hiyo, nakuomba Mheshimiwa Waziri, tujiulize ni wapi tumekosea ili tuweze kuwa werevu kwa muda wa kutosha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikirudi kwenye Mkoa wangu wa Katavi, tuna mkakati wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Katavi, naomba sana Halmashauri ya Manispaa ya Katavi kwa jitihada zake yenyewe imeanzisha mkakati huo wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Katavi pamoja na mazonge zonge mengi yanayoendelea, naomba Mheshimiwa Waziri watu hawa ambao wamekwishatenga eneo, kwanini na nyie kama Wizara msiwa-support wananchi hawa ambao wameonesha initiative?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu, nami naomba sana, ikiwa Mheshimiwa Rais Kikwete alitoa zawadi ya Chuo Kikuu cha Dodoma kwa Mkoa huu wa Dodoma na nchi kwa ujumla wake, namwomba na Rais wangu Mheshimiwa Dkt. Magufuli, auangalie Mkoa huu wa Katavi, ni mikoa ya pembezoni kwa ukweli. Nami niseme, uwepo wa Chuo Kikuu ni fursa. Maeneo ambayo yana vyuo, yanaibua mambo mengine! Watu wanaokwenda huko kwa ajili ya kusoma na kufanyaje, wanaibua fursa nyingine katika maeneo hayo. Kwa hiyo, naomba sana nikianzia na hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoke hapo niende kwenye Chuo chetu cha VETA, ni Chuo cha siku nyingi, lakini miundombinu imekuwa ni chakavu. Nakuomba Mheshimiwa Waziri tukiangalie, Chuo kile kimejengwa kwa siku nyingi, kinahitaji tu kuboreshewa miundombinu. Nikitoka hapo niende pia kwenye shule kongwe. Nalisema hili kwa sababu ukurasa wangu wa saba umesema ukarabati wa shule kongwe, umetaja shule saba. Nakuomba Mheshimiwa Waziri, kuna shule ya watoto wa kike ya Mpanda Girls. Shule ile haina uzio, ni dada zetu na inapelekea watu wanaanza kuvamia maeneo ya shule. Ufumbuzi pekee ni kuwatengenezea fensi; na nikitoka hapo, ni kweli pamoja na huduma ya maji ili wale dada zetu waendelee kufanya vizuri.
Mhesimiwa Mwenyekiti, baada ya kutoka hapo kwenye suala la Chuo Kikuu na Mpanda Girls, naomba nizungumzie kidogo suala la maslahi. Mimi naamini katika historia. Historia ni somo ambalo linatufunza wapi tumetoka, wapi tulipo na wapi tunakwenda. Kipindi cha nyuma ilikuwa ukiona mtu amevaa vizuri, anamiliki pikipiki au anamiliki baiskeli, ujue ni Mwalimu. Kipindi cha nyuma! Kwa hiyo, mtu ambaye alikuwa nadhifu, amekaa vizuri, ana maslahi mazuri, ni Mwalimu. Kama historia inatuambia tumetoka wapi? Tuko wapi na tunakwenda wapi? Kwanini tusirudi kwenye history, tukaangalia past ili ituangalie tuko wapi kwa maana ya sasa hivi na baadaye tunakwenda wapi? Tutapata ufumbuzi. Habari ya maslahi ya Walimu wakaaje, wafanywaje, tujifunze tu, huko nyuma tulikuwa tukifanyaje? (Makofi)
Vilevile Mheshimiwa Waziri, kwa maana ya elimu nilikuwa naomba nizungumzie habari ya maktaba ya Mkoa wa Katavi naomba sana eneo hilo. Kwa upande wa Chuo Kikuu, naomba nikizungumzie Chuo Kikuu Huria. Nimeona kuna mkakati wa makusudi wa kuviboresha Vyuo vya maeneo mengine lakini kwa eneo langu la Katavi niseme tena kuhusu habari ya Chuo Kikuu Huria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hatuna chuo chochote. Chuo pekee ambacho kiko kule kwa sasa hivi, ni Chuo Kikuu Huria. Kwa hiyo, nilikuwa naomba miundombinu hiyo ya Chuo Kikuu Huria tuweza kuiboresha ili watu hawa ambao kwa ukweli watoke pale kwenda katika maeneo mengine kwa ajili ya kufuata huduma za shule, waweze kuipata katika eneo ambalo liko jirani na wao. (Makofi)
Eneo la elimu bure, niseme kitu kimoja, naishukuru Serikali kwa hili. Jamani suala hili ni mchakato, nimewahi kusema huko nyuma. Ukiwa umepika chai, habari kwamba chai ina sukari nyingi, una uwezo wa kuongeza maji; au habari kwamba chai haina sukari, unaweza kutafuta sukari. Kwa hiyo, kwanza tumeanza na elimu bure, lakini kwa kutoka hapo tutaendelea kuboresha kwa kadiri mahitaji yanavyohitajika. La msingi ni kwamba tumeanza. It is a process, ni mchakato! Siyo suala la mara moja ukamaliza. Kwa hiyo, naipongeza Serikali, lakini na wazazi tusisahau wajibu wetu wa msingi, kuna maeneo ambayo wazazi wana nafasi yao ya kuendelea kuchangia, tusiiachie tu Serikali peke yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikitoka hapo, naomba suala zima la study za kusoma kwa maana ya Kuandika Kuhesabu na Kusoma (KKK) lizingatiwe sana. Hilo litaendelea kutusaidia kuwafanya vijana hawa katika hatua ya awali. Ni aibu leo hii kuzungumza kwamba kuna mwanafunzi amepita shule, halafu hajui kusoma, hajui kuandika, hajui kuhesabu. Ili kukidhi mahitaji ya hilo, eneo la ukaguzi limekaaje jamani? Kwa sababu kama kuna eneo la ukaguzi, tutafikaje kusema huyu hajui kusoma? Au huyu hajui kufanyaje! Maana yake kuna sehemu tumekosea. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri tuboreshe maeneo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja, nashukuru.