Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naridhia hizi itifaki zote ambazo tunataka kuzipitisha hapa, lakini nataka nijikite kwenye hiyo ya Montreal, Itifaki ya Montreal. Hii ni itifaki muhimu sana na ninaamini kama ingekuwa dunia haikupitisha hii saa hizi tungekuwa tunazungumzia hali mbaya sana kwa afya zetu kuhusiana na jinsi ambavyo tabaka ya ozone ambayo ingeshakuwa imeharibika kwa kiasi kikubwa sana. Itifaki hii sasa hivi inaendelea kulenga kuboresha kanda zetu au nchi mbalimbali jinsi ambavyo inajiwekea sasa mikakati zaidi ya kuhakikisha kuwa inaendelea kuzingatia utekelezwaji wa itifaki hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwetu sisi Tanzania ni muhimu sana kwa sababu tumeona kabisa jinsi ambavyo matatizo ya tabianchi yanatuathiri, na athari zinazotokana na mmomonyoko au ubomokaji wa ozone layer ni mbaya kuliko hata zile tunazozizungumzia za masuala ya carbon dioxide. Kwa hali hiyo nafikiri protocol hii ni muhimu sana kuizingatia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala langu ni moja tu kwa Serikali; itambuliwe kuwa huko nyuma utafiti uligundua kuwa hii ozone au hili tabaka linaathirika sana na kemikali zinazotumika katika kutengeneza viyoyozi, kutengeneza majokofu na kutengeneza haya makopo ya dawa za kupulizia. Na hivi karibuni tumeona kuwa majokofu na viyoyozi vingi chakavu vinaingia nchini, sijui ni nani anayekagua kuhakikisha kuwa havibebi zile kemikali ambazo huko nyuma ndiyo zilitambulika kuwa zinaathiri hili tabaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kuwa kutokana na hii, hii gharama ya kuondoa, ya kusafisha hizi kemikali zilizoko katika matumizi ya wananchi ni kubwa sana. Huko nyuma kulikuwa kuna fungu lilikuwa linatolewa ambalo lilikuwa linapitishwa Umoja wa Taifa, nakumbuka kwa Tanzania Umoja wa Taifa walikuwa wanasimamia fungu hilo, kwa hiyo walikuwa wanafanya kazi na viwanda kuhakikisha kuwa wanaondoa hizi kemikali. Sasa sijui kwa sasa hivi kama lile fungu bado linaendelea kwa Tanzania.