Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Machano Othman Said

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

MHE. MACHANO OTHMAN SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uhai na uzima, na pia niwapongeze sana Waheshimiwa Mawaziri wote wawili kwa kuwasilisha maazimio haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitazungumzia hili Azimio la WTO. Kwanza naunga mkono uamuzi wa Serikali wa kulileta hapa Bungeni, lakini pia naomba Waheshimiwa Wabunge tulipitishe azimio hili kama maazimio mengine ambayo tumeyapitisha Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, azimio hili lina umuhimu mkubwa kwa Tanzania katika uendelezaji wa biashara, lakini pia kuzalisha bidhaa bora. Ni vyema kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanya mashauri na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili, pamoja na kwamba Bunge linaridhia azimio hili, lakini pia kwa upande wa Zanzibar nao waelewe na wafahamu faida ambazo zitapatikana kwa kuridhia azimio hili kwa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri alipowasilisha alieleza faida za azimio hili kwa kuzitaja baadhi ya ibara ambazo zitaleta na kuimarisha mshikamano na mtengamano wa kibiashara kwa Tanzania. Kwa mfano Ibara ya 10 inatoa fursa kwa kuweka forodha ya pamoja na mambo mengine ambayo yatasaidia katika uendelezaji wa biashara, lakini pia kulinda na kuimarisha wataalam wetu katika shughuli za uzalishaji na kuweka viwango bora vya uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vyema kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na kwamba tulichelewa kidogo kwa sababu kati ya nchi nyingi tu sisi tulikuwa miongoni mwa nchi 18 ambazo zilichelewa kuridhia azimio hili, lakini leo ni furaha kwamba tumekubaliana na tumeridhia azimio hili. Hivyo kama ulivyozungumza, hatutakiwi kuzungumza sana isipokuwa kuunga mkono azimio hili, na mimi naliunga mkono kwa asilimia mia. (Makofi)