Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante nami kwa kupata nafasi hii niweze kuchangia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipende tu kuipongeza Kamati na Mwenyekiti wa Kamati ya PAC ni Mujumbe wa PAC. Nitaongelea suala la TBA (Wakala wa Majengo Tanzania).

Mheshimiwa Naibu Spika, TBA ilipewa jukumu la ujenzi wa majengo kujenga Taasisi mbalimbali za Serikali nchini Tanzania na mkataba wenye gharama ya shilingi bilioni 24,068,482,278. Pesa hii ni ndogo sana ukilinganisha na mradi wenyewe jinsi ulivyo na kutokana na uhaba wa pesa iliyotolewa wkamba ni ndogo tunaona miradi mingi ya TBA inasuasua. Mapungufu yamekuwa mengi sana. Kutokana na hilo pia hata bill of quantity haikufuatwa. Kwa hiyo, kama haikufuatwa BOQ kumefanya gharama za mradi kutojulikana hadi sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya serikali kutoa bilioni 24 tunaona kabisa ni jinsi gani miradi hii inayosimamiwa na TBA haifanyikazi kwa ukamilifu kwa sababu unakuta msimamizi mmoja wa mradi ana miradi miwili. Aende huku akasimamie mradi, atoke huku aende akasimamie mradi huu kwa hiyo unakuta mradi huu mwingine ambao anakuwa ameuacha unakua umesimama anaporudi kwenye huu mradi mwingine na huu nao unasimama. Na pia inabidi achukue vifaa hivi anavyotumia kujengea kwenye mradi huu mwingine, mradi (a) aende akachukue tena akajengee kwenye mradi (b) kwahiyo tunakuta kuna upungugfu mkubwa sana wa ufanisi wa kumaliza miradi kwa ufasaha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano; jengo la Makao Makuu ya Tume hapa Dodoma, TBA ilikuwa inafanyakazi pale kujenga lile jengo matokeo yake wameshindwa na baada ya kuona kwamba lile jengo halitaisha kwa wakati ikabidi sasa wachukuliwe SUMA JKT kwenda kumalizia ule mradi pale na hadi sasa SUMA JKT ndiyo bado inaendelea kujenga ule mradi ambao ulikuwa unasimamiwa na TBA.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaenda pia upande wa NHC; upande wa NHC miradi mingi nayo imetelekezwa yaani haieleweki kwamba hii miradi itakwisha au laa! Mfano; mradi ule wa Kawe 711; ule mradi una thamani ya shilingi bilioni 142. Bilioni 142 ni pesa nyingi sana lakini cha ajabu mradi unatelekezwa. Pesa ambayo imetolewa haijafanyakazi yoyote. Kwa kweli inakuwa ni kitu ambacho kinailetea hasara Serikali yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukaguzi wa CAG ulibaini pia ongezeko la gharama la shilingi bilioni 6.86 pesa ambayo haikutolewa maelezo yoyote hadi leo hii. Tunaomba tuelezwe kinagaubaga pia tuelewe kama Kamati hii bilioni 6.86 imetoka wapi na kwa sababu haikutolewa maelezo yoyote kwa hiyo hatujui mpaka sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu kwa Serikali ni kwamba; iwe inatoa pesa kwa wakati. Itakapokuwa inatoa pesa kwa wakati, majengo yale yatakamilika kwa wakati na value for money itaonekana.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na nashukuru kwa kupata nafasi hii. (Makofi)