Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Kwanza kabisa napenda kuwapongeza Ofisi ya TR kwa kazi nzuri wanaoifanya pamoja na Kamati ya PIC lakini pia Ofisi ya Mheshimiwa Spika kwa sababu wamekuwa bega bega na sisi kuona kwamba tunapeleka ufanisi kwenye Mashirika yote ya Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi zipo nyingi lakini kwa kwenda haraka ningependa kwenda moja kwa moja kwenye mada na nitapenda nichangie mashirika mawili, nitapenda nichangie shirika la TAWA ambalo linahusika na uhifadhi wa Wanyamapori lakini pia nitapenda nichangie Kampuni ya Kilombero.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAWA ilianzishwa kupitia Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Na.5 ya mwaka 2009, lakini pia katika kifungu cha 8 ilimpa mamlaka Mheshimiwa Waziri kuweza kuunda chombo chenye mamlaka kamili katika kusimamia na kuhifadhi wanyamapori. Hata hivyo, mpaka leo hapa ninapoongea takwa hili la kisheria halijatimilika na Kamati yetu inasema kwamba kuna umuhimu kabisa wa kuona TAWA wanapatiwa sheria yake kwa maana ya kwamba tunaamini kabisa tutakapopata sheria yake TAWA itaenda kujiendesha kwa mapato tofauti na ilivyo sasa. Tunasema kwamba ni wakati mahususi TAWA iweze kujipatia sheria yake kwa sababu tumeona kazi kubwa TAWA inayofanya. Hapa ninapoongea ardhi tengefu zote zaidi ya asilimia sitini katika nchi yetu zinasimamiwa na TAWA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo haitoshi, ninapoongea hapa kwa mfano mapori tengefu yote yanasimamiwa na TAWA, lakini pia mapori ya akiba, wetland, open areas zinasimamiwa na TAWA, Ramsar sites zinasimamiwa na TAWA lakini pia utalii wa baharini unafanyika na TAWA na vitu kadha wa kadha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema sasa ni muda mahususi TAWA iweze kupatiwa sheria yake kwa sababu kwa muda mfupi toka ianze kufanya kazi mwaka 2016, TAWA ilipata mtaji kutoka Ngorongoro wa shilingi milioni mia tatu hamsini, lakini ninapoongea hapa leo TAWA imeweza kutengeneza faida ya shilingi ya bilioni 48 kwa mwaka. Kwa hiyo, hii ni positive move na tuna-recommend kwamba tunaomba sasa Serikali ione umuhimu wa kukipatia chombo hiki sheria yake mahsusi ili kiweze kujiendesha chenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majukumu haya na record nzima walizoliweka TAWA pia kwa namna ambavyo walivyojianzisha wenyewe walikuwa na magari machache sana na Mkurugenzi kwa kipindi hicho alikuwa anatumia gari ya TANAPA kufanya operations za taasisi. Hadi sasa ninapoongea, TAWA ina magari 77 brand new zero kilometer, kwa hiyo haya ni mafanikio makubwa kwa muda mfupi wa miaka mitatu. Kwa hiyo, tunasema kwamba ni muhimu sasa Serikali ikaamua kugatua madaraka pamoja na operations zote ziende TAWA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na haya tunaposema TAWA ipewe majukumu yake, tunafahamu kabisa, kwa mfano Sheria Na.5 kifungu cha 8 ambacho kinamtaka Waziri atoe mamlaka kamili ya chombo hiki ni kwamba kwa sasa katika sheria hii ilivyo, Mheshimiwa Waziri ndiye mwenye mamlaka ya kutoa vitalu vya kitalii vya uwindaji. Haya ni makosa, tutakapopata sheria hii mamlaka haya yataenda kwenye Board of Directors, lakini pia Kamishna wa TAWA atakuwa na mkono wa moja kwa moja kusimamia haya kwa sababu atakaposimamia na kuweza kutoa mwenyewe vitalu, tunaamini kabisa ataenda kuhifadhi sustainable management kwa taasisi hii ya TAWA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoongea hapa hata utalii wa picha Mheshimiwa Kamishna wa TAWA anakuwa hana mamlaka kamili, ingawaje jukumu hilo liko katika taasisi yake lakini hasimamii yeye, suala hili linasimamiwa na Mkurugenzi wa Wanyamapori.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaomba kabisa Wizara husika pamoja na Serikali ione kuna ulazima kabisa wa kuipa TAWA sheria yake ili iweze kushindana kama tunavyoona TANAPA inavyofanya vizuri, Ngorongoro inavyofanya vizuri, tukiipatia TAWA sheria yake na Meja Jenerali Semfuko alivyokuwa imara, tunaamini kabisa TAWA itaenda kufanya wonders katika hii dunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia nichangie suala la Kilombero. Ni dhahiri kama walivyosema wajumbe wenzangu, kwa sasa tuna umuhimu kabisa wa ku-support suala hili na tunaomba Serikali iwe makini na isimame na sisi katika kuona kwamba kibali kili walichoomba hawa watu toka miaka miwili iliyopita, basi kitolewe kwa sababu domestic demand ya sasa ya sukari ni tani 550, lakini kwa sasa tuna tani laki tatu na elfu hamsini katika viwanda vyetu vya ndani. Kwa hiyo, tunajua kabisa tuna gap, hivyo, ni vizuri sasa tukakubali kiwanda hiki kipanuliwe kwa sababu kitakapopanuliwa, sasa hivi Kilombero Sugar inachangia shilingi bilioni 350 katika uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika plan hii ya expansion itaenda kuchangia bilioni 700, lakini pia wafanyakazi wataenda kuongezeka kutoka elfu nane mpaka elfu kumi na saba. Uchakataji wa malighafi katika taasisi ile unasema kwamba asilimia sitini ya raw materials ambayo ni miwa itazalishwa na out growers ambao ni mama zetu, dada zetu, vijana waliokuwa disparate walikosa ajira, wamezagaa kule Morogoro, ardhi ni nzuri, maji yapo, kwa hiyo, tunaomba kabisa Serikali itilie mkazo jambo hili kwa sababu sisi wabeba ilani tunayo ya kujibu, suala la ajira bado ni kizungumkuti, lakini ardhi tunayo, maporomoko ya maji tunayo na kiwanda kipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo nyuma mpaka Waziri alilazimika kwenda kiwandani pale kwa sababu kulikuwa na migomo mingi sana, wakulima wadogowadogo kila wakipeleka miwa wanaambiwa mara sucrose haipo, mara hivi, watapewa terminologies zote zile ili mradi tu kuonesha kwamba hawahitaji miwa mingi kwa kiasi hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaamini tutakapokwenda kupanua kiwanda kile malighafi tunayoambiwa asilimia 60 ya malighafi itatoka kwa wakulima wadogo wadogo, kiwanda kitachukua yote kwa sababu sasa hivi wakienda wanapewa terminology ngumu, lakini hii ni kuonesha kwamba kiwanda walichonacho kwa sasa hakiwezi ku-accommodate mazao yote ambayo yanapatikana katika muktadha huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo mengi ya kuzungumza katika hili, lakini nafikiri kwamba ni vizuri sana Serikali ikaona umuhimu wa kupanua kiwanda hiki, kwa sababu hata kama tunataka tuipe Mkulazi ambayo ni taasisi ya Serikali pengine, na-assume hivyo, labda tukiisaidia Kilombero sisi tutakosa stock yetu. Hapana, leo ukienda Mkulazi tumewapa ardhi, tumetoa wafungwa magereza wamekwenda wamelima, wamesafisha, tumefanya kila kitu, lakini Mkulazi haina uwezo, leo miwa ya Mkulazi inaachwa kule porini, imetelekezwa kwa sababu hata kiwanda hakijanunuliwa, kinu hakipo, tuwape wawekezaji ambao wako tayari. Hakuna nchi ambayo inakataa au hakuna nchi ambayo haikubali uwekezaji wa watu binafsi na sisi pia naamini hatupo huko na kwa kuwa hatupo huko, naomba sasa Serikali ione umuhimu wa ku- accommodate hawa wenzetu, tuwape kibali ambacho wamekisotea kwa miaka miwili leo ili waweze kuanza kufanya upanuzi huo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haya machache narudia tena, napenda kuipongeza Kamati yangu kwa kazi nzuri iliyofanya. Natambua kabisa katika mashirika tuliyoyahoji, kipaumbele chetu cha kwanza kilikuwa ni kuona kwamba Bodi za Wakurugenzi zinakuwepo, baadhi ya taasisi nyingi, asilimia 70 tulizokutana nazo ambazo zilikuwa hazina bodi sasa hivi zina bodi. Pia nafasi za kukaimu; asilimia 72 ya nafasi zote zilizokuwa zinakaimishwa, sasa hivi wameenda kupata substantive post, lakini, siyo hivyo tu, Kamati yetu pia ilisimama kikamilifu kuona kwamba na wanawake wanapewa nafasi katika mashirika haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo awali wakati tunaanza shughuli zetu za uendeshaji wa shughuli yetu tulikuja kubaini wanawake wengi wanaachwa kwenye ngazi za maamuzi, kwa hiyo kupitia Mheshimiwa Chegeni alikuwa imara sana kuweza kuona kwamba shirika linakuwa na namba nzuri ya wanawake wanaosimama katika ngazi za maamuzi. Kwa kweli katika hili naipongeza sana Kamati yangu, kwenye suala la gender tulisimama vizuri, Mheshimiwa Chegeni nampongeza mno pamoja na nafasi yake aliyonayo alisimama kikamilifu kuwatetea akinamama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haya machache nakushukuru sana na naomba kuunga mkono hoja taarifa zote za Kamati kama zilivyosomwa na kuwakilishwa. (Makofi)