Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia hizi Kamati mbili na niwapongeze Wenyeviti wote wa Kamati. Nianze kwa kutazama tu jambo la mazingira na niishauri sasa Serikali yetu huko tunakokwenda sasa kuwa na Wizara maalum ya Mazingira ambapo nchi zilizoendelea sasa zina Wizara hii ya mazingira na ndiyo Wizara maarufu katika nchi zote za Ulaya na nchi zingine, kwa mfano Brazil ndiyo Wizara maarufu sana; ukienda Kenya ndiyo Wizara maarufu sana ya mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa sababu hili tunaloliona leo ambapo tunazungumza habari ya mafuriko au habari ya kiangazi ni matokeo ya climatic change, ni climatic crisis ambazo tunaziona sasa hivi hapa na kwa bahati mbaya kitengo hiki cha mazingira hakiko kwenye viwanda, kinazungumziwa kama kitengo tu. Hata ukitazama hapa results zake ni kama vile watu wa ushauri, lakini huko kwenye maeneo ya nchi zote duniani hata Tanzania hapa kilitakiwa kuwa kitengo cha kuamua nini kifanyike katika nchi yetu kwa sababu nchi yetu sasa tunakokwenda suala la mazingira ni muhimu sana kuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ukiangalia katika maeneo kama ya Bunda kwenye Jimbo langu barabara ya Maliwanda, Stephen Wasira yote imekatika, barabara ya Kandege Tingilima haipo, barabara ya Sarawe, Kambubu haipo, Sarawe Bukama, barabara ya Kambubu Sarawe nayo haipo, barabara ya Nyangere Unyali haipo, barabara ya Nyabuzume Kiloleli haipo, barabara ya Tingirima na Tiling‟ati na Nyamso haipo, zote zimekatika; na hii yote ni kutokana na kwamba maeneo maalum ya hizo barabara, aidha watu wamelima mpaka kwenye barabara au watu wameng‟oa viti yote milimani au mabonde yote yameziba kwa hiyo hakuna mahali ambapo watu wanaweza kupita kwenye maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nilikuwa nafikiri kwamba ni vizuri sasa tunakokwenda hii Wizara ya Mazingira tukaipa kipaumbele sana kwenye mambo kama haya ili yaweze kutusaidia huku tunakokwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie uwanja wa Musoma, uwanja wa ndege Musoma Mkoa wa Mara; Mheshimiwa Rais alifanya ziara toka wa tarehe 4, mpaka tarehe 8 Septemba, 2018 na akazungumza sana juu ya ujenzi wa uwanja wamusoma, lakini mpaka leo hatua hazijaenda vizuri na uwanja haujajengwa tunasikia tu ten million imetolewa uthamini yakinifu umefanyika lakini hakuna kitu kinachoendelea pale. Tunazungumza habari ya reli ya kutoka Tanga, Moshi Arusha, Musoma kila mwaka tunaiona kwenye bajeti hapa lakini mpaka leo toka Mwalimu Nyerere amekuwepo mpaka leo sisi hatujawahi gari moshi linafika kwenye Mkoa wa Mara. Kwa hiyo, nafiri kwamba ni wakati muafaka sasa wakati tunashughulika na maendeleo haya yaende kwenye Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kusoma taarifa hapa nimeona kuna taarifa ya matrekta yaliyokuwa yananunulia na Serikali kupitia shirika letu la Suma JKT na Kampuni ya US, Russi ya Poland ambayo inaonekana asilimia 65 hela zimetolewa kwenda kununua matrekta, na matrekta 825 ndiyo yamefika kati ya 2,400 yaliyokuwa yanatakiwa kufika hapo. Sasa najiuliza katika haya matrekta yaliyokuja ni asilimia 34 point je, matrekta yaliyobaki hela zake zimelipwa au hazikulipwa? Na hiyo asilimia 65 ya hela zilizotoka zimekidhi vigezo matrekta yaliyokuja au kuna mengine hayajaja, na mbaya zaidi wanasema katika shirika hilo ambalo tumefanya makubaliano nalo linaelekea kufilisika sasa najiuliza hizi hela za wakulima ambazo tunatakiwa kuleta matrekta kuwasaidia wakulima zitapotelea humo au hatua gani itachukuliwa. kwa hiyo nilikuwa nashauri Serikali katika hili uweze kifanya vitu vya haraka zaidi kwenda kuona kinachoweza kutokea katika suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Bunda kuna barabara ya inatoka Makutano Butiama, Sanzati barabara sasa ina miaka nane toka inatengenezwa na kila mwaka wanapewa muda wa kumaliza lakini wameshindwa kumaliza naomba Wizara inayohuka Wizara ya Miundombinu ichuke hatua kwenye barabara ya Makutano Sanzati ambayo inatengenezwa kwa miaka 6 sasa, kuna barabara ya kutoka Nyamswa kwenda Bunda barabara ya lami, Mheshimiwa Rais amefika pale tarehe 6 akasema Mkandarasi aanze mara moja hatujamuona mpaka leo, kuna barabara ya kutoka Sanzati kwenda Nata Mgumu, tumetangaziwa kuwa Mkandarasi yuko barabarani hajafika mpaka leo. Kwa hiyo, tunaomba Wizara inayohusika ili iweze kuchukua hatua hizo za kuweka Wakandarasi kwenye barabara ambazo zinaweka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka nizungumze hayo kwenye Jimbo langu, lakini nilishukuru Bunge kwa ujumla kwa hatua ambayo ilikuwa inazungumziwa asubuhi, kwamba katika maisha yetu ya kitanzania na katika watanzania wote mambo muhimu ya kuzingatia ni usalama wa nchi yetu na maendeleo ya nchi yetu. Kwa yoyote yule ambaye anayumbisha nchi yetu na ikiuletea giza kwenye mambo yake ya kule anakotaka yeye hatua kali zichukuliwe dhidi yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sakata linaendelea huku Marekani la impeachment trial, watu wenginine wanafikiri kwamba pengine hilo linatokana na sijui Ukraine au kuzungumza jambo fulani lakini ukweli ni kwamba kwa mara ya kwanza katika Marekani uchaguzi wao 2016 uliingiliwa na Urusi, na wanajiuliza mara mbili mbili waliingiaje mpaka leo, nani aliwaruhusu kuingia lakini leo Marekani wanazungumza kuingiliwa uchaguzi wao, lakini wao toka mwaka 1948 wamekuwa wakiingia nchini zingine uchaguzi kwa mfano uchaguzi wa Italia wa mwaka 1948 wameingia na kuweka na mgombea wao, uchaguzi wa Israel, mwaka 1996 Criton amekwenda pale ameweka mtu wake kuwa Waziri wa Israel.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaomba huko tunakokwenda nchi yetu ijue kwamba wakoloni hawatakuja hapa, lakini mipango Marais wanaowataka vibeberu wao itakuwepo. Kwa hiyo tuchukue hatua za kutosha kwenye jambo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)