Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwamba nimemaliza adhabu yangu vizuri na nimerudi nimewakuta hamjabadilika sana. Kwa hiyo, nawashukuru sana wale waliosaidia kupata adhabu ya muda mrefu, mmehuisha sana roho yangu na thamani yangu kupenda haki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni Bunge la mwisho. Maana yake mwaka huu Bunge hili lote tutaondoka twende kwenye uchaguzi na kwa miaka mitano ambayo tumekaa hapa ndani ya Bunge, Bunge hili kama limefanya kazi ya kusaidia nchi zaidi ya kuipamba Serikali ni kwa kiwango kidogo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajadili taarifa za Kamati, Viwanda na Biashara. Taifa lolote linalotaka kuimarisha biashara katika nchi yake, kitu cha kwanza ni utawala bora uonekane kwa macho na siyo tu utawala bora; leo utawala bora, utawala wa sheria, demokrasia katika Taifa hili imeonekana siyo sehemu ama siyo part ya mafanikio ya nchi. Juhudi kubwa sana zinafanyika za kuondoa Wapinzani katika uchaguzi unaofuata. Jambo hilo linaweza likafanikiwa, lakini halitafanikiwa na baraka za vizazi vya Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetoka kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa; ule uchaguzi hayakuibiwa matokeo, uliibiwa mchakato. Mchakato uliibiwa na CCM imeshinda kwa asilimia 100. Mnapiga makofi, mnafurahi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakwenda kwenye Uchaguzi Mkuu Mwaka 2020; kuna commitment kubwa sana ya kuhakikisha kwamba hakuna Mpinzani atakayerudi. Unapoongelea biashara na viwanda, wawekezaji wanaangalia utawala bora ili kuleta biashara ambazo ni sustainable. Unapoongelea viwanda na biashara wawekezaji na watu wa ndani wanaangalia utawala wa sheria uliothabiti ili kuleta mitaji na kuongeza mitaji katika kujenga uchumi wa nchi. Kwa hiyo, ili ku-improve biashara katika Taifa hili na ku-improve viwanda, kitu cha kwanza cha kuimarisha ni utawala wa sheria ambao mtu yeyote hatautilia mashaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, factors za utawala bora katika kuamua uchumi wa nchi ni namba moja. Leo Kenya inawawekezaji wengi kuliko Tanzania. Kenya haina rasilimali nyingi kama Tanzania, lakini wawekezaji wana-confidence na Kenya kwa sababu hata Mahakama za Kenya za ndani zina uhuru wa kutosha wa ku-handle matter za wawekezaji kuliko hata Mahakama za nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Kenya inapokea watalii wengi kuliko Tanzania, leo Kenya ina vitanda ziada kuliko Tanzania karibu vitanda 30,000 ni kwa sababu ya mazingira ya utawala wa kisiasa wa nchi ile. Mheshimiwa Uhuru leo na Raila wanashikana mikono pamoja kujenga Taifa lenye umoja. Leo Kenya huwezi kujua tofuati ya mpinzani na Serikali kwa sababu wameamua kujenga nchi. Hapa Mpinzani ni Mhaini. Hata akitoa maoni, yanakuja maazimio ya AG; yamekuja maazimio leo hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ningekuwa Serikali, suala la Mheshimiwa Zitto ningelipuuza tu, kabisa! Leo Mheshimiwa Zitto ameandika barua tarehe 22 Januari, maazimio ya World Bank kuhusu mtafaruku wa Sera na Serikali ya Tanzania ni mwaka juzi 2018. Barua ya tarehe 22 Janauri ya kimkakati leo mmeishikia Bango, yanatolewa maamuzi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaambiwa aangalie kama kuna kosa la jinai katika maoni aliyotoa Kiongozi wa Upinzani wa Chama cha siasa. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mimi nachnagia Taarifa ya Kamati ya Viwanda na Biashara na hoja yangu ni moja tu, ya kwamba ili kuwepo na biashara ambazo ni sustainable, tunahitaji utawala bora. Sasa mimi ni Mbunge, naishauri Serikali kwamba kwa suala ambalo limetokea leo Bungeni, ambalo wala mtafaruku wake siyo Mheshimiwa Zitto, Zitto anaweza akawa amedandia, mtafaruku wake ni confusion ya policy kati ya Serikali na World Bank.

Sasa ndiyo nikasema, ningekuwa ni mimi, badala ya kuamuru Mheshimiwa Zitto atiwe hatiani, ningesema Mheshimiwa Zitto apuuzwe halafu Serikali mwendelee kujadili na World Bank mfikie consensus. Hiyo ndiyo ingekuwa Utawala. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa maana yake Mpinzani anapotoa maoni sasa internationally naye anatiwa kibano, mnatia mashaka wale watu ambao wanataka kuleta mitaji mingi hapa. Hivi vitu vinakwenda internationally na vikienda Kimataifa watu wanasema ile nchi Bwana, hata Mbunge akitoa maoni huwa anapewa money laundering, tusubiri kwanza tuone utawala upite.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo letu siyo tu kuwatoa madarakani, hata mkibaki madarakani, lakini tukiona Taifa hili linakuwa ni mahali salama pa kuishi, hiyo ni baraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaongea biashara; leo…

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Tusikilize taarifa. Iwe ni taarifa ya kujenga.

T A A R I F A

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wakati ilitolewa hoja kiwekwe kipimo, ile alcoholic nini ile, hapo. Ninafikiri kuna haja ya kukirudisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme nini? Ninachowaambia Waheshimiwa Wabunge na Serikali, leo huko mitaani sisi tunafahamu hali ya kibiashara ilivyo mbaya. Tunafahamu jinsi ambavyo watu wanaondoka, ambavyo mitaji inahama na hiyo ni kwa sababu ya mashaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TRA hata wakiongeza kodi kwa kiwango gani, lakini kama Taifa halina uncertainty, bado kodi huwa haiendi kwa yule anayefanya biashara, inakwenda kwa mlaji wa mwisho. Sasa kuna mashaka makubwa. Leo kupata working permit nchi ama business permit, mimi niko Arusha, watu wengi wameondoka kwa sababu ya working permit. Wamekuja Wazungu wanataka kufanya miradi wanaondoka kwa sababu ya working permit. Mimi najiuliza, mtu anakuja na investment ya labda shilingi milioni 10, una…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.