Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumshukuru sana Mwenyezi Mungu, lakini pia niishukuru kamati kwa kusoma taarifa yao vizuri ambayo imesheheni mambo ya msingi na kwa sehemu kubwa imetushauri sisi tunaohusika na suala la mazingira. Yako baadhi ya mambo machache ambayo naweza kuyatolea ufafanuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kamati imehitaji ili tujiimarishe zaidi katika usimamizi wa suala la mazingira. Ni kweli ziko changamoto ambazo zinajitokeza kwenye mzingira kulingana na wakati tulionao. Tumefanya maboresho ya sera yetu ya mwaka 1997, ili iweze kuendana na wakati uliopo sasa, ili iweze kutatua changamoto zinazojitokeza kwenye suala la mazingira, ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, lakini pia, bio teknolojia:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kamati imegusia suala la ufinyu wa bajeti; nilitaka nilieleze tu Bunge lako kwamba, kulingana na ongezeko la mapato ya ndani sasa tunafanya mawasiliano na wenzetu wa Wizara ya Fedha, ili tuweze kuongezewa fedha, lakini jambo jingine kukwama kwa Mfuko wa Taifa wa Mazingira. Nakubaliana na kamati kwamba, huu ndio muarobaini wa matatizo ya mazingira ambayo yanajitokeza na ulikwama na sasa tunatengeneza waraka maalum kulingana na sheria yetu ya mazingira ya mwaka 2004, ili kuhakikisha kwamba, tunapeleka waraka huu kwenye mamlaka zinazohusika na kuweka ufanisi wa mfuko huu wa mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine ni uelewa mdogo juu ya mambo ya mazingira:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yetu imeendelea kufanya kazi hii kwa kina zaidi, kwenye vyombo vya habari, lakini pia kwenye semina, midahalo mbalimbali na tutaendelea. Tunaishukuru kamati kuendelea kutukumbusha juu ya suala la uelewa wa mazingira bado ni mdogo kwenye jamii yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine ni vyuma chakavu, biashara ya vyuma chakavu ambayo sisi tunazungumzia suala la udhibiti wa taka hatarishi, tumetengeneza Kanuni ya Mwaka 2019 ya Usimamizi wa Udhibiti wa Taka Hatarishi na kanuni hii imeanza kazi rasmi. Kwa hiyo, nilitaka niwatoe hofu wafanyabiashara wa biashara hii ya vyuma chakavu kwamba, Wizara imeweka utaratibu maalum kushirikiana na Wizara ya Fedha, lakini kushirikiana na Wizara ya Viwanda na vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha tunalinda miundombinu yetu ya ndani isiweze kuharibiwa kupitia biashara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kamati imezungumzia urasimu wa kutoa vibali:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, yawezekana ni kweli, lakini jambo hili tumelichukua kama lilivyo tuende tukakae na wataalam wetu kuweka njia iliyo sahihi kuondoa urasimu uliopo. Tunatambua tumetengeneza, tumebadilisha kanuni, lakini tunatambua pia, katika suala la vibali leo tunatoa Provision License Clearance, tunatoa vibali vya muda mfupi ndani ya siku saba mtu anapata kibali wakati anasubiri kibali cha tathmini ya athari ya mazingira. Kile cheti cha athari ya mazingira kinachukua muda mrefu na ndio maana inawezekana wawekezaji baadhi wanaona kama vibali hivi vina urasimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tunao wataalam elekezi nao tumeboresha kanuni yao. Wataalam elekezi ambao wanatambuliwa na Baraza la Hifadhi ya Mazingira kwamba, tumeboresha kanuni yao na kanuni yao itaanza kazi rasmi mwaka huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye hoja ya Mheshimiwa Mbunge Mwita Getere,Mheshimiwa Mwita Getere amezungumza vizuri na ushauri wake tumeupokea kama Wizara kwamba, sasa ifike mahali Wizara ya Mazingira isiwe mambo mengi yanafanywa na Wizara za kisekta. Mheshimiwa Mwita Getere ametoa ushauri kwamba, sasa Wizara ijitegemee kufanya mambo hayo, ili kukabiliana na changamoto kubwa inayojitokeza. Na sisi tunakubaliana na hilo na tunalichukua kwa ajili ya kulifanyia kazi, ili tuone huko tunakokwenda tuboreshe maeneo ambayo tunaona yana changamoto, ili Wizara hii isiendelee kukabiliana na changamoto hizi na matokeo yake inaleta kutokuwa na ufanisi ndani ya Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekekelezaji wa agizo la kupiga marufuku mifuko ya plastic:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kamati imeeleza vizuri. Na kwa ushirikiano mkubwa wa kamati mifuko ya plastic leo nchini kwa sehemu kubwa sisi hatuitumii, lakini wako wafanyabiashara wababaishaji wanaopitisha mifuko hii kwa njia za panya, lakini iko mifuko ambayo haizingatii viwango na wenzetu wa TBS wameshatoa viwango na mifuko inahitaji kuwa na standard.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.