Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Jumanne Kibera Kishimba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kahama Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. JUMANNE K. KISHIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naungana na Wabunge wenzangu kuchangia Wizara hizi mbili za Kilimo, Uvuvi na Maliasili. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Rais, Mawaziri na Watumishi wote wa Wizara zote hizi. Naipongeza Wizara Kilimo hasa kwa suala kuondoa bei na indication price kwenye mazao yote itatusidia sana hasa kwenye mazao yetu ya pamba ambayo yalikuwa yana tusumbua sana wakati wa kutao bei na mara bei zinapoanguka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala hili la soko la mazao limeendelea kuwa tatizo kubwa sana. Kwa hiyo tunaomba Wizara ya Kilimo na Wizara ya Viwanda na Biashara zijaribu namna yoyote kuendelea kuwabana wenye viwanda hasa vya pombe na viwanda vingine waweze kutumia mali za Tanzania kwenye pombe au bidhaa ambazo sio za nje.

Mheshimiwa Spika, maana yangu ni kwamba kuna bia kama za balimi, kuna bia kama za eagle ambazo watumiaji ni watanzania ambazo watumiaji ni local. Vizuri wenye viwanda na Wizara Kilimo na Wizara ya Biashara ijaribu kuwabana ili kuwasidia wakulima wetu kupata bei za mazao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka jana nilikuja na suala la bangi, bahati nzuri nchi zingine mbili ukiondoa Uganda, Zambia na Malawi wameruhusu. Na vizuri mwaka 2015 Bunge lako hili lilipitisha nitaisoma sheria hiyo. Kifungu cha 12 cha Drug control and enforcement act. Cha 2015 kinaipa DCEA mamlaka ya kuruhusu ulimaji, usafirishaji wa bangi, mirungi, micocoa OPM kwa ajili yamatumizi ya tiba.

Mheshimiwa Spika, bei ya bangi duniani imepanda mara dufu na nchi zote zinazozunguka zimekwisha ruhusu. Wakati wa majumuisho tunaomba Mheshimiwa Waziri wa Kilimo… (Makofi)

SPIKA: Hii ni hoja muhimu sana naomba tuisikilize. (Makofi)

MHE. JUMANNE K. KISHIMBA: Mheshimiwa Spika, naomba Waziri wa Kilimo kwa kuwa sheria hii ipo, aje atupe ufafanuzi kwamba watu wanaotaka kulima wamuone nani na imetungwa na Bunge hili mwaka 2015. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, waliopiga marufuku bangi ni wazungu miaka ya 40. Lakini wazungu wale wale wamegundua ndani ya bangi kuna dawa. Na sisi wenyewe tunaenda kwenye viwanda vya dawa. Je sisi tuki-import dawa yenye material ya bangi tutakuwa tuna-import toka wapi? Na tunatai-declare na namna gani?

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI: Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Waziri Kairuki taarifa.

T A A R I F A

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, naiona hoja ya Mheshimiwa Kishimba, lakini nipende kusema kwamba tayari hata sisi wizarani tumeshapata wawekezaji kama wawili wambao wameonyesha nia ya kuwekeza katika kilimo lakini pia kuchakata mafuta bangi kwa ajili ya matibabu. Tunaendelea kulifanyia kazi kama Serikali kwa sababu hakuna bado miongozo kifungu cha 12 kimeeleza kama itakubalika au laa! Ni hatua zipi na utaratibu gani uweze kufuata.

Kwa hiyo, nimuuombe Mheshimiwa Mbunge atuachie kama serikali na mamlaka zinazohusika tuendelee kulichaka na pindi litalopokuwa tayari basi majibu yatatolewa. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Kishimba taarifa hiyo.

MHE. JUMANNE K. KISHIMBA: Mheshimiwa Spika, taarifa yake naiunga mkono, labda chakuomba kwa kuwa bei ya masoko ni bei ya ushindani ni vizuri Serikali ifanye uamuzi huo mapema zaidi.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Musukuma taarifa.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru nilikuwa napenda kumpa taarifa mzungumzaji kwamba kikawaida Bunge linapotunga sheria kinachofuata ni kanuni. Nilikuwa nafikiria Mheshimiwa Waziri angetuambia kanuni zipo tayari ili tuanze kulima maana bangi itaporomoka bei.

SPIKA: Mheshimiwa Kishimba endelea.

MHE. JUMANNE K. KISHIMBA: Mheshimiwa Spika, sisi Tanzania kwa record kwa Afrika ni nchi tatu kwa kulima bangi ya magendo. Sasa kama wataruhusu na sheria kama ilivyo inaweza ikatusaidia sana kuongeza mapato na kuondoa magendo. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani yupo hapa kama anaweza kutoa msamaha hata kwa bangi iliyopo kwa miezi 6 kama msamaha anavyotoa wa silaha wananchi wakawasilisha bangi hizo polisi watu wakauziana polisi na TRA wakapata fedha na wanunuzi wakaja kununua hapa. Inaweza ikasaidia watu wetu wakapata pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni vizuri wakati dunia inapobadilika lazima twende haraka sana, Uganda wamepewa hii AU zaidi ya dola ya milioni mia tano kwa ajili ya kilimo cha bangi wanatoa udongo toka Malaysia. Lakini sisi bahati nzuri wakulima wetu wana utalaamu wa kulima bangi muda mrefu. Kwa hiyo, kama serikali itapitisha na hiyo sheria kwa kuwa ipo, basi tumuombe Mheshimiwa Waziri wakati wote kama atapitisha iwe mapema kabla bei haijaporomoka. Ahsante sana nashukuru sana.

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Spika, Mwongozo wa Spika.

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge bado dakika za Mheshimiwa Kishima zipo pale. Lakini niwahakikishie this is not a joke anachochangia. Nilikuwa Canada majuzi hapa kwenye Mkutano wa Maspika wa Commonwealth duniani, ni big business in Canada, big, big business. (Makofi)

Kwa hiyo, anazungumza kitu cha msingi sana wala sio utani. Eeeh tena linaweza likawa zao moja kubwa kabisa la biashara linaloweza kuongoza kuliko mazao mengi tu, kabisa likafanya mapinduzi makubwa sana ya kipato. Kwa hiyo, anachokizungumza Mheshimiwa Kishimba hazungumzi bangi itumike vile ambavyo tunafahamu hapa nchini. Tunazungumzia habari ya kilimo moderated, monitored na utaratibu wote halafu wanapelekewa wanaohitaji kwa ajili ya kutengeneza madawa ya wanyama na binadamu. Malizia Mheshimiwa Kishimba dakika zako.

MHE. JUMANNE K. KISHIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa hiyo tulikuwa tunaomba sana Wizara ya Kilimo wajaribu kulifikilia kama ulivyosema kwamba hii bangi sasa ni tiba. Kama ni tiba na sisi tunaagiza material kutoka nje na dawa kutoka nje ambazo zina bangi.

Ni vizuri sasa kutumia bangi yetu na huenda tukawa wazalishaji wazuri zaidi maana yake watu tayari wanao uzalishaji wa bangi. Na inaweza ikasaidia Wizara ya Afya kupunguza na kupunguza gharama za pesa tunazoagiza toka nje.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri wa Uwekezaji amelisema vizuri kwamba na yeye lipo mezani, tunaomba wenzetu wa Zambia na Malawi wananchi wamelalamika kwamba baada ya kuwa imeruhusiwa, wameruhusu matajiri peke yake.

Tunaomba kama wataruhusu basi na wakulima wetu wadogo wadogo wapewe nafasi hizo ili na wao waweze kujipatia chance kwenye muda huu ambao zao hili litakuwa kwenye soko. Badala ya kuyapa makampuni makabwa peke yake ya nje ni vizuri na wakulima wadogo na watu wadogo wadogo wakaruhusiwa ili wote ku-enjoy bahati ambayo itatokea duniani. Ahsante sana. (Makofi)