Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii adhimu niweze kuchangia taarifa ya Kamati hizi mbili. Nitajikita zaidi kwenye Kamati ya Kilimo, Kamati ambayo nilidumu kwa takriban miaka miwili na nusu.

Mheshimiwa Spika, nianzie na suala la korosho. Msimu uliopita huu wa 2019 hakukuwa na malalamiko mengi ya wakulima wa korosho kucheleweshewa kulipwa fedha zao, ingawa bei ime-drop tofauti na msimu uliopita ule wa 2018, lakini malipo yalikwenda kwa haraka. Changamoto ni msimu wa 2018.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri yupo hapa, anajua, wako wakulima mpaka leo wanadai fedha zao. Mpaka sasa nilitegemea taarifa ya Kamati inge-include kwamba ni kwa kiwango gani ama ni kiasi gani ambacho wakulima bado wanadai hawajapatiwa fedha zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakumbuka taarifa ya mwaka 2019 ya Kamati hii ya Kilimo ilielezea na iliitaka Serikali kuhakikisha wanakamilisha malipo ya wakulima kwa wakati. Kwa hiyo, naomba sana Wizara ihakikishe kwamba deni la msimu wa 2018 wanalimaliza. Taarifa zilizopo ni kwamba information ambayo Waziri anayo, ile amount ambayo wakulima walikuwa wanadai na Serikali ikatoa, namshukuru Mheshimiwa Rais alitoa zile fedha, lakini zile information inaonekana hazikuwa sahihi, kuna fedha nyingi zaidi ya shilingi bilioni 10 ambazo hawa wakulima waliachwa, hawakuwa included. Kwa hiyo, hii ndiyo leo ukienda pale Mtwara unakuta wakulima wa korosho siku zote wanaenda Mtwara, wanarudi wanaambiwa tutawalipa pesa ikipatikana.

Mheshimiwa Spika, imefikia hatua wakulima waliouza korosho 2019 wamekatwa fedha zao wakiambiwa kwamba tuliwalipa shilingi 3,300/= mwaka 2019 kwahiyo tunazikata hizi fedha kwenda kuwalipa wakulima wengine ambao hawajalipwa, lakini mpaka sasa malipo hayajafanyika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba sana, kwa kuwa Waziri yupo, Naibu Waziri yupo, wajitahidi kuhakikisha wanakamilisha kulipa deni la mwaka 2018. Kuna wakulima wengi ninaowafahamu, wapo wanadai na kila siku wamekuwa wakisumbuka kwenda Mtwara kufuatilia fedha zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lipo zao la nazi, nimekuwa nikisema sana hapa zaidi ya mara mbili mara tatu. Zao hili liko hatarini kupotea na ni zao ambalo kwa mikoa ya Pwani wale Waswahili tunaotokea Pwani ni kama identity yetu. Identity ya miji yetu, inapendezesha miji yetu lakini pia ni kwa wapenzi wa chakula ambacho kimeungwa na nazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unajua, utafiti unahitajika kufanyika kwenye zao la nazi. Minazi mingi sasa hivi ukienda Kisiju imekufa, hukuti ile minazi ya zamani sasa hivi. Ukienda Pangani, the same story, ukienda Lindi minazi mingi pale eneo la Ng‟apa ambalo ndilo eneo linategemewa kutoa nazi nyingi, inakufa na nimekuwa nikisema mara nyingi sana. Kuna wakati nilizungumza na Mheshimiwa Naibu Waziri pale ambaye sasa hivi yuko Utumishi wa Umma nilimwambia niko Jimboni nimewakuta wakulima wanalia minazi inakufa. No research tujue kwamba kitu gani kinapelekea minazi kufa ili ufanyike utafiti tuweze kutibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama ujuavyo, mtu wa Pwani akila ubwabwa au wali ule bila nazi, hauendi kabisa. Tunaomba sana ufanyike utafiti wa kina ili ijulikane tatizo ni nini?

Mheshimiwa Spika, jambo lingine, mvua zinanyesha, kwa hiyo, ilikuwa ni wakati muafaka sasa hivi wananchi kuhakikisha wanavuna maji. Maji ya mvua yangeweza kutumika kwenye kilimo cha umwagiliaji lakini pia hata matumizi ya kawaida. Wakiulizwa swali hapa Wizara ya Maji, unakuta kila Mbunge anasimama kuonyesha kwamba kwake kuna shida ya maji. Mwaka 2019 tulipitisha Sheria ya Maji hapa. Sheria ile inataka uvunaji wa maji, mtu akivuna lita 20,000 awe analipa kodi. Ukiangalia lita 20,000 ni kidogo sana kwa matumizi.

Mheshimwa Spika, nilifikiria Kamati ingekuja na mapendekezo, kwa sababu haya niliyaona nikiwa Mjumbe wa Kamati hii, wananchi na wadau walikuja kulalamikia kwamba sheria hii inaweza ikakwaza watu wenye malengo ya kutaka kuvuna maji ya mvua. Mvua Mwenyezi Mungu ametujalia kama mwaka huu mvua ipo ya kutosha sana, lakini shida ni hiyo kwamba sheria inataka ukishafikisha kutaka kuvuna lita 20,000 ambayo ni maji kidogo sana, uweze kulipa kodi, uitolee taarifa Wizarani na mambo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napendekeza sheria hii ingefanyiwa marekebisho. Kamati ingekuja na mapendekezo sheria hii kuifanyia marekebisho kuongeza wigo na ku-encourage watu waweze kuvuna maji ya mvua ili tupunguze hili tatizo la watu kulalamikia maji, maji maji.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, niliamua nichangie kwenye Sekta hii ya Kilimo. Ahsante sana. (Makofi)