Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na mimi niweze kuchangia mawazo kidogo kwenye Wizara ya Kilimo, Maliasili pamoja na Maji. Nadhani hii ni karibuni mara ya kumi nimekuwa nikizungumza jambo moja katika Mkoa wangu wa Katavi asilimia 90 ya wananchi wa Mkoa wa Katavi wengi ni wafugaji pamoja na wakulima lakini ukisoma hotuba ya Kamati zote mbili hususan kilimo pamoja na Maliasili hizi ni Kamati ambazo zinaingiliana kwa baadhi ya mambo. Changamoto kubwa walioieleza Kamati ni pamoja na migogoro na manyanyaso yanayoendelea kwa wakulima pamoja na wafugaji katika taifa hili. Sasa kwa ujumla wake manyanyaso hayo pamoja na uonevu umekuwa ukifanyika katika mikoa ambayo ina wafugaji wengi na wakulima wengi.

Mheshimiwa Spika, lakini wiki mbili zilizopita jambo la aibu Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika pamoja na Mkurugenzi wa Tanganyika walipokea pesa ya rushwa shilingi milioni 60 walimchaji mfugaji mmoja alikuwa na ngombe zaidi ya 600 wakawa wanamtoza milioni moja kwa ng‟ombe mmoja.

Sasa sheria inasemaje; mambo haya tukiwa tunalalamika watu wanaona kwamba tunalalaika kila siku lakini tunachokisema katika Taifa hili katika Mkoa wa Katavi naweza nikasema katika Wilaya ya Tanganyika inaongoza kwa rushwa chini ya huyu Mkurugenzi anaitwa Lumuli pamoja na Mhando, huu ni mwaka wa nne nazungumzia mambo haya.

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, wizi, rushwa zimekidhiri katika Wilaya ya Katavi.

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, tunapokuwa tunazungumzia mambo haya...

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Rhoda kuna taarifa nilimsikia Mheshimiwa Msongozi

T A A R I F A

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, nimemsikia mchangiaji anayeendelea kuchangia akizunguza suala la Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi kwamba wamepokea rushwa ya shilingi milioni 60. Kwa hiyo, nataka mchangiaji atueleze anaweza kutoa ushahidi kwa jambo hili analolizungumza?

SPIKA: Mheshimiwa Rhoda.

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, naomba niendelee na mchango wangu kwa sababu hata Mheshimiwa Jacqueline anayoongea haishi Mkoa wa Katavi wala haelewi kinachoendelea katika Mkoa wa Katavi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka niongelee uonevu na unyanyasaji unaofanyika na Mkuu wa Wialaya huyu huu ni mwaka wan ne na si hayo tu, Mheshimiwa Waziri alikuwepo juzi wiki tatu zilizopita anaelewa wizi wa pesa zilizopigwa na huyu Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi anaelewa. Sasa Serikali imechukua hatua gani kuwawajibisha huyu Mkuu wa Wilaya ambaye kwetu kule ni mzigo watu hawamtaki kwa sababu amekuwa ni chanzo cha migogoro sio solution. Badala ya kumsaidia Mheshimiwa Rais amekuwa ni tatizo na anatamba kule yeye ndio Mfalme sasa kule yaani ndio Mungu mtu wa Wilaya ya Tanganyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, watu hawamuhitaji kutokana na kwamba amekuwa ni chanzo cha migogoro na sio solution kwenye Wilaya ya Tanganyika. Nataka Waziri akija atueleze ni sheria ipi ilitumika kuchaji ng‟ombe mmoja milioni moja na sheria inasema ni shilingi 30,000 kama ni ng‟ombe akiingizwa kwenye eneo la hifadhi. Sasa Mamlaka haya ya halmashauri ya Tanganyika wameyatoa wapi na wamechukuliwa hatua gani, Mheshimiwa Waziri akija atueleze wizi huu wa pesa zilizopigwa na huyu Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi, solution yake ni nini.

SPIKA: Mheshimiwa Rhoda unasema ni wamechaji milioni moja kwa ngombe mmoja?

MHE. RHODA E. KUMCHELA: Mheshimiwa Spika, ndio ng’ombe mmoja

SPIKA: Yesu na Maria na huyo Mkuu wa Wilaya ni nani?

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, Mkuu wa Wilaya anaitwa Muhando na Mkurugenzi anaitwa Rojazi Lomoli.

Mheshimiwa Spika, nataka nizungumzie vijiji 920 Mheshimiwa Lukuvi alikuwepo kwenye ziara ya Rais iliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana lakini tulitangaziwa kwamba kuna vijiji 920 vilivyorasimishwa kutoka kwenye maeneo ya hifadhi wananchi wapewe kwa maana ya uhaba wa maeneo ya malisho.

Mheshimiwa Spika, sasa mpaka hivi tunavyoongea si Mkoa waKatavi peke yake mpaka na maeneo mengine baada ya kauli hizi ambazo Mheshimiwa Rais alitamka kwamba haitaji kuona wafugaji wanateseka katika Taifa lakini imekuwa ni vice versa. Wafugaji wamekuwa wakipigwa ukienda kwenye Kata ya Stalike watu wanapigwa lakini Rais alitoa kibali watu waendelee kuishi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Asante sana Mheshimiwa Rhoda dakika tano zimeisha.