Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

MHE. LUCY M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuchangia Taarifa za Kamati hizi tatu.

Mhesheshimiwa Mwenyekiti, ni Mjumbe katika Kamati ya Utawala na TAMISEMI, tulijadili mambo mengi sana katika Kamati na hoja nyingi zimewasilishwa na Mwenyekiti wetu wakati anatoa Taarifa, naomba nisisitize mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ni miundombinu inayoelekea kwenye Chuo cha Hombolo, barabara ya Ihumwa-Hombolo; hali ya barabara ile ni mbaya sana na ni ya muda mrefu na wakati wataalam wanatengeneza wamekuwa wakitengeneza kwa changarawe. Naiomba Serikali badala ya kutengeneza kwa changarawe basi watengeneza barabara ya lami kusudi isilete tena usumbufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni uhaba wa watumishi; karibu sekta zote kuna kilio cha uhaba wa Watumishi. Nikitoa mfano katika hospitali ya Mkoa ya Njombe, watumishi wanaotakiwa ni 320 lakini hadi sasa waliopo ni 149. Kwa kweli inakua ngumu sana katika kutekeleza kazi sawa sawa na kama tunavyojua kwamba upande wa afya tunahangaika ili kupunguza vifo vya wakinamama lakini tunapokua na Watumishi wachache namna hii itakuwa ni vigumu sana kupunguza vifo vya wakinamama. Niiombe Serikali kwasababu tunaenelekea kwenye kipindi cha Bajeti, basi itenge Bajeti ya kutosha kusudi kuweza kuwaajiri Watumishi wa kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia Watumishi hao hao ni miaka takribani minne sasa na huu ni wa tano hawajaongezewa mishahara yao. Niiombe Serikali iwaongezee kishahara kwa sababu tunaelekea kipindi cha Bajeti sasa basi iwafikirie hao Watumishi kuongezewa mishahara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala langu lingine ni Utawala Bora; Utawala Bora ni pamoja na kuwapa watu au wananchi uhuru wa kutoa mawazo yao. Tumeshuhudia watu wanatoa mawazo yao lakini wanakamatwa. Mfano; kuna Mwanafunzi wiki mbili zilizopita huko UDOM alipiga picha kwenye ndoo za maji kulalamikia tatizo la maji, mwanafunzi yule alikamatwa. Niiombe Serikali itoe uhuru wa wananchi kutoa mawazo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala lingine ni suala la Utawala Bora; wananchi wana haki ya kuchangua viongozi wanaowataka lakini pia kuchaguliwa. Nimeshuhudia toka kipindi cha chaguzi ndogo za Ubunge na Udiwani na hatimaye Serikali za Mitaa. Wananchi wamelazimika kuwa na viongozi wasiowapenda ndiyo maana hadi sasa hivi ukienda maeneo mbalimbali wananchi wanawagomea wale viongozi waliowekwa, wanasema hawataki kuongozwa na hao wenyeviti. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wote tunaabudu na tuna dini zetu. Kila mtu ana imani yake. Tuliapa hapo mbele kwamba tutasema ukweli kwamba yale tutakayoyatekeleza yatakuwa ni kulingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sasa nimeshuhudia tunafanya kinyume kabisa. Hata dhamira yangu kama Mkristo, mimi dini yangu ni Mkristo, wakati mwingine najisikia vibaya kwamba sisi Wabunge sio wakweli. Naomba tuishauri Serikali yetu, pale inapokosea tuikosoe ni pamoja na kuisisitizia Serikali kuwa na Utawala Bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali, kwa sababu imekuwa haizingatii matakwa ya Katiba, itunge Katiba mpya, pia kuweka Tume huru itakayosaidia kutatua haya mambo ambayo yamejitokeza huko nyuma hasa kipindi hichi cha uchaguzi. Kwa sababu tunaenda kipindi cha Uchaguzi Mkuu, isije ikatokea kama ilivyotokea huko nyuma. Ninaomba sana, kila mtu atafakari, kama kweli unamwabudu Mungu wako, basi ikuguse hiyo kwamba tunahitaji kuwa na haki, tutende haki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi/Vigelegele)