Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kukushukuru lakini kuzipongeza Kamati zote tatu kwa kazi nzuri waliyoifanya kuwasilisha hapa Bungeni na naziunga mkono taarifa za Kamati zote tatu kwa namna walivyowasilisha na kufanya kazi na kutoa taarifa ya mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAMISEMI ni chombo ambacho kinasimamia asilimia kubwa sana utendaji wa Serikali nampongeza sana Mheshimiwa Jafo na Mawaziri hawa Wawili anaofanya kazi nao pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli ni Wizara ambayo ndiyo ni engine ya Taifa hili, yako masuala ya Elimu, Afya na masuala mengi na hasa mazingira hata sherehe yetu ya mazingira asilimia kubwa ya kazi zetu zinafanywa na Watendaji wa halmashauri ambao wako chini ya Mheshimiwa Jafo na Wizara yake ya TAMISEMI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawapongeza sana lakini nichukue nafasi hii vilevile kuunga mkono kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kubuni vitambulisho vya Wajasiriamali sasa hivi suala la Wamachinga, Mama lishe katika Mkoa wa Dar es Salaam na Mikoa yote Tanzania usumbufu hakuna tena. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais wakati anafunga Kampeni yake pale Dar es Salaam mwaka 2015 alisema atahakikisha anapiga marufuku mgambo na kweli mgambo wote wamepigwa marufuku na hakuna mgambo yoyote anayesumbua wafanyabiashara wadogo wadogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyabiashara wadogo wadogo sasa na mitaji midogo waliyokuwa nayo wanahakikisha kuwa mitaji yao iko salama na mali zao haziibiwi wala hawadhurumiwi tena. Hii yote ni kutokana na vitambulisho hivi ambavyo Mheshimiwa Rais amewapa vijana wake na wao waone ni sehemu ya Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kuwapongeza wote waliofaulu katika shule zetu za Sekondari kwa mara ya kwanza katika Mkoa wa Dar es Salaam sasa hivi baada ya kutoka division zero sasa hivi wanafunzi wameanza kupata division one na hakuna division zero. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii yote ni jitihada ya Mheshimiwa Rais, Wizara ya Tawala na Serikali za Mitaa kuweka Elimu bure na kuboresha Elimu katika shule zetu. Tumejenga mabweni shule ya Jangwani sababu wanafunzi waweze kusoma na walale kwenye mabweni wasirudi majumbani nampongeza sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Jafo Wizara hii unaitendea haki wewe na Manaibu Mawaziri wako Wawili baada ya maneno hayo naunga mkono Kamati zote tatu. (Makofi)