Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nianze utangulizi wangu nikijikita sana kwenye Mambo ya Nje. Dunia iligundua kwamba kuna nchi zina nguvu sana. Tuki-apply dhana ya sovereignty of the state kuna baadhi ya nchi inaweza ikaziumiza nchi nyingine. Kwa msingi huo, ikaja dhana ya kidiplomasia, kwamba hawa watu watatumia ushawishi, uwezo, mahusiano kuweza kufanya nchi hizi ziweze kuishi na kufanya kazi pamoja.

Mheshimiwa Spika, nimetoa utangulizi huo kufuatia mambo yanayoendelea kati ya Tanzania na Marekani. Secretary of the State alitoa kauli kuhusu mwenendo wa nchi yetu kwenye mambo ya demokrasia, haki za binadamu na mambo mengine. Akaeleza, tusipokuwa makini, tunaweza tukaharibu mahusiano yetu na Marekani na matokeo yameanza kuonekana.

Mheshimiwa Spika, sasa anapotokea Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi yetu anajaribu ku-confront statement ya Marekani kwa kutishia kwamba watatufanya nini na tukitaka tutarudisha watu wao. Hiyo siyo diplomasia na huo siyo msingi wa diplomasia duniani.

Mheshimiwa Spika, hili narudia. Tuliposema tunahitaji Waziri wa Mambo ya Nje aliyebobea kwenye diplomasia, tulimaanisha mtu mwenye ushawishi, mtu mwenye uwezo wa kuimarisha mahusiano ili Tanzania, nchi masikini tuweze kuimarika kiuchumi na kuweza kutekeleza bajeti zetu kupitia donor community. Sasa hili inabidi tuliangalie kwa umakini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka jana, 2019 mwishoni, Tanzania iliyopewa heshima ya kuwa Makao Makuu ya the African Court on Human and People’s Rights tumetishia kama siyo kujitoa, maana zimetoka kauli mbili za Mawaziri. Mheshimiwa Prof. Kabudi anasema tumejitoa, Mheshimiwa Mahiga anasema hatujajitoa, tumeomba wabadilishe protocol.

Mheshimiwa Spika, nchi yetu iliyopewa tangu enzi za uhuru, AICC hapa Tanzania, tuna hii Mahakama ya Afrika, siyo kwa bahati mbaya. Kwa hiyo, kusema tunajitoa kwenye AICC, kusema tunataka kujitoa kwenye the African Court on Human and People’s Rights, ni kujaribu kuona ile heshima tuliyopewa hatukustahili.

Naiomba Serikali, tunayo haja kubwa ya kuimarisha diplomasia katika nchi yetu. Hili siyo jambo la kufanyia mizaha kwa sababu kurudisha heshima tuliyopewa, zipo nchi nyingi sana zinajaribu na wamekosa fursa hiyo.

Mheshimiwa Spika, niseme kidogo kuhusu ndugu zetu walioko China, waliopata ugonjwa wa coronavirus. narudia tena, kazi ya kwanza ya Serikali ni kulinda, kuhudumia na kuhakikisha watu wake wapo salama. Sasa leo Mbunge anasimama Bungeni, anauliza swali mahususi: Tanzania itafanya hatua gani kuhakikisha watu wake wanarudi nchini salama? Serikali inasema, watu wabaki huko huko kwanza, haya mambo mengine tutashughulikia pole pole.

Mheshimiwa Spika, hili Bunge ni la wananchi. Serikali kazi yake ni kulinda ustawi wa wananchi na kulinda usalama wa wananchi. Tunahitaji kauli thabiti ya Serikali kuhusu evacuation process.

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Salome, kuna taarifa.

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Nimekuona Mheshimiwa.

T A A R I F A

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba tu nimkumbushe Mheshimiwa Salome kwamba tamko la kusema raia wa Tanzania ambao wapo nchini China ilikuwa ni kwa manufaa yao. Tumeshuhudia Serikali ya China ikiwashauri wananchi wao wenyewe wa Jamhuri ya Muungano wao wa China waendelee kukaa ndani kutokana na maambukizi au mfumo wa maambukizi wa ugonjwa ule. Kwa hiyo, kubaki kwao ndani kuweza kufanya movements za kutoka kwenye miji yao kuja mpaka Tanzania kunawaweka kwenye hatari zaidi kuliko kuendelea kuwa china.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

SPIKA: Mheshimiwa Salome, pokea ushauri huo.

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika kwa kulinda heshima ya kiti chako, uliielekeza Serikali hapa wiki iliyopita walete kauli, walete mpango wao wa evacuation kwa ajili ya ndugu zetu wanaoishi China. Leo ni Jumatano, watu wetu wanaishi kwa hofu, wazazi wao walioko Tanzania wana hofu. Hivi hii ni serikali gani isiyojua hili? Tumeelezwa kwamba Marekani wameshaanza evacuation process, watu wanarudishwa, Ujerumani wanarudisha watu Tanzania…

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika Taarifa.

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Tanzania watu wetu wanaishi kwa hofu na wale ni Watanzania wenzetu.

SPIKA: Mheshimiwa Salome, kuna taarifa unapewa. Nia ni kukusaidia tu Mheshimiwa Salome kupitia taarifa hiyo. Mheshimiwa Waziri Nchi, tafadhali.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika, hatugombani katika jambo hili ambalo lina maslahi ya Watanzania na nchi kwa ujumla. Kwa hiyo, Mheshimiwa Salome ajue kabisa kwamba hatugombani katika jambo hili.

Mheshimiwa Spika, utakumbuka ndani ya Mkutano huu wa Bunge Mheshimiwa Waziri Mkuu hapa alishatoa maelezo, lakini Waziri mwenye dhamana ya Wizara ya Afya alishatoa maelezo yakinifu. Sasa tunachotaka kufanya hapa kwa muktadha wa jambo hili ambalo ni lenye afya tu, Mheshimiwa Salome anapaswa kushauri zaidi kuliko kulalamika ama kuishutumu Serikali haijachukua hatua zozote.

Mheshimiwa Spika, ili kuthibitisha kwamba Serikali imefanya kazi yake ipasavyo, ndiyo maana Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa tamko, Waziri wa Afya ameendelea kutoa tamko na hiyo yote ni Serikali. Hatulali, tunaendelea kulifanyia kazi jambo hilo. Kwa hiyo, tuko tayari kupokea ushauri, lakini siyo tuhuma kwamba Serikali haijajali wala kushughulikia suala hilo.

SPIKA: Unapokea taarifa hiyo?

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, hiyo taarifa siipokei. Hivi unafikiri Bunge lako linajua Watanzania wangapi wanaumwa? Watanzania wangapi huenda wameshapoteza maisha? Watanzania watarudi tarehe ngapi mwezi wa ngapi hapa nchini? Marekani wamesharudisha watu wao nchini. Hii Serikali ya Chama cha Mapinduzi inayojitapa ina ndege, itumie ndege hizo nane waweke moja Watanzania warudi nchini kwa maslahi ya Taifa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana. Dakika zako zimekwisha.

MHE. SALOME W. MAKAMBA: …na kwa ajili ya kuleta amani katika nchi yetu. Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)