Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya mimi kuchangia jioni ya leo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizishukuru Kamati zote mbili ambazo zimewasilisha hapa taarifa zao, zimefanya kazi vizuri, zimetuonesha Wabunge kwamba kitu gani kinafanyika kwenye Kamati zao lakini kipekee nimshukuru Waziri wa Nishati Dkt. Kalemani ambaye kwa kweli ni mtambo wa bidii, kijana anayetembea kijiji kwa kijiji, hatua kwa hatua, transfoma kwa transfoma, nguzo kwa nguzo, nyaya kwa nyaya, anafanya kazi nzuri sana tunapaswa hata tulete pongezi hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuwapongeze kwa kazi pamoja na Naibu wake na watumishi wake wote kwa kazi nyingine zinazofanywa na Mawaziri hapa iko siku tufanye kama mlivyofanya juzi kwenye Maspika waliokuja hapa tuanze kuwapa tunzo Mawaziri wanaofanya kazi vizuri humu ndani kwani sisi tuna kosa gani. Mawaziri wanaofanya kazi vizuri kwa mwaka kama huu tunaomalizia tunawapa vyeti au tunawapa zawadi maalum hata tukisema siku moja wachukue posho yetu ya siku moja sio mbaya, wanaofanya kazi vizuri. Kwa hiyo Waziri wa Nishati anafanya kazi nzuri sana na Naibu wake na watendaji wake wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Waziri wa Ulinzi kwa kweli sijui tunasemaje, katika watu ambao nimewahi kuwaona wanashinda vishawishi vya binadamu hapa duniani wakiwa hai ni Waziri Mwinyi, anafanya kazi vizuri sana. Ameshinda vishawishi vya binadamu na tama za binadamu anafanya kazi vizuri sana. Nimpongeze Mheshimiwa Doto kijana huyu kama tunamtunza vizuri na tunampa moyo atakuwa kiongozi bora katika nchi hii, ana nidhamu ya kutosha, anafanyakazi vizuri, lakini pia nimpongeze pacha mwenzangu Waziri Lugola ambaye ajali imempata kazini, amefanya kazi vizuri huku nyuma, ametufanya sisi Wabunge leo tukitembea barabarani trafiki wanapisha uongo au kweli?

WABUNGE FULANI: Kweli.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Kwa hiyo, amefanya kazi, kwa ajali iliyompata ni ajali tu, aendelee kuhangaika na ajali yake lakini alifanya kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Waziri mwenzake aliyekuja alinde yale maslahi ambayo tunaona yapo kwa Wabunge. Pale ambapo tunakamatwa tunafanyaje tukipiga simu apokee haraka. Kwa hiyo niwapongeze wote kwa kazi nzuri waliyofanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba Bunge hili katika orodha ya Mabunge, maana yake watu huwa wanasahau, Bunge hili katika orodha ya Mabunge yaliyopita, hili Bunge ni la mfano. Limemsaidia Mheshimiwa Rais kufanya kazi kubwa sana za Kitaifa na lazima tuandikwe kwenye historia.

Mheshimiwa Spika, Bunge hili ndiyo limeleta Bwawa la Nyerere, limetengeneza barabara za flyover, limesaidia Rais kuleta Hospitali za Mikoa, Hospitali za Wilaya na limetoa elimu bure. Kwa hiyo, Wabunge walioko hapa wote kwa ujumla hata wanaopiga kelele hapa na wenyewe wanaandikwa tu. Maana kelele hapa ni za Bungeni tu, wakienda mitaani kule wanasema nimeleta umeme, nimeleta hospitali, nimeleta hiki. Hawa hawa ndio wanapiga kelele humu ndani. Wakiambiwa wapige kura hapa, wanapiga hapana. Wakienda huko wanajivunia maendeleo ya Chama cha Mapinduzi. Hawana kingine wanachoweza kujivunia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tarehe 9 Machi, 2017, Rais wa Marekani anaitwa Donald John Trump alimpongeza Rais wa Tanzania. What is so special? Kwa sababu ni Rais bora wa Afrika, alimpongeza Trump. Watu wajue sera zetu za Chama cha Mapinduzi za nchi yetu ya kutofungamana na upande wowote ziko pale pale. Hii habari ya kusema sijui nini kimefanyika huko, sijui Pakistani twende, sijui jambo limetokea tukio mahali twende, sijui nani amesema hivi; hatuendi huko! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi ni nchi ambayo inajitegemea, ambayo haifungamani na upande wowote. Watu waje, Marekani ni marafiki zetu. Wakija na upande wa ushoga, hatutaki ushoga. Tutakataa! Maana nawashangaa watu, tunakuwa kama vile mazoba fulani hivi. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, juzi Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amekataa hadharani. Sasa kama kweli hoja yetu ni kukubali ushoga ili tuwe na maadili bora ya nchi hii, hatuwezi sisi mambo ya namna hiyo! Kama ni ushoga, waende kwa wanaoutaka ushoga uko! Sisi hatuwezi kuwa na ushoga. Wanaoutaka ushoga waushabikie. CCM na viongozi wake na Wabunge wake, hatutaki ushoga. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, sasa nije kwa ndugu yangu Dkt. Kalemani. Naomba Dkt. Kalemani sasa tuelewane na hapa sasa nitaongea pole pole. TANESCO umetembea sana kwenye vijiji, lakini bado uzalishaji wa accessories wanaita viunganishi ni tatizo kwenye nchi yetu. Bado mita ni tatizo kwenye maeneo yetu, bado nguzo kwenye viwanda, Wakandarasi wanaenda kulipa fedha, hawapati nguzo kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, bado TANESCO hawajawa vizuri bado, isipokuwa TANESCO Mara kwangu wamekuwa vizuri. TANESCO hawajawa vizuri, hawawezi ku-react haraka kwa watu. Kwa hiyo, tunaomba sasa, kwa kuwa umefanya kazi kubwa sana ya kutembea ardhini, sasa rudi ofisini uwashughulikie wale ambao hawafanyi kazi vizuri ili tuweze kufanya kazi vizuri kwenye maeneo haya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, juzi Mheshimiwa Rais amesema soko lile liitwe Ndugai, lakini najiuliza, tuna jengo la Utawala hapa linaitwa Annex, liko hapo, lina jina gani? Kwa nini Mheshimiwa Rais akuone huko akupe, sisi Wabunge hatuwezi kusema Annex ya Utawala apewe Ndugai? Kuna utata gani hapa? Mimi mbona sioni shida hapa!

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi natoa pendekezo, Annex iliyoko hapo iitwe Ndugai, kwani kuna ubaya gani? Amefanya kazi kubwa sana ya Serikali hapa.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)