Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kufuta Hasara itokanayo na Maduhuli ya Madeni ya Nyuma ya Ada na Leseni za Magari, Riba na Adhabu kwa kipindi kinachoishia tarehe 30 Juni, 2019

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kufuta Hasara itokanayo na Maduhuli ya Madeni ya Nyuma ya Ada na Leseni za Magari, Riba na Adhabu kwa kipindi kinachoishia tarehe 30 Juni, 2019

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa nafasi hii. Pia nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa kuleta Azimio hili la kufuta bilioni 398. Hii siyo mara ya kwanza kufuta deni, nimwombe Mheshimiwa Dkt. Mpango aliridhie ombi langu ili kusudi kuondoa haya mawazo ambayo yanawapelekea wenzetu kufikiri kwamba Chama cha Mapinduzi kinategemea hizi pesa ili kusudi kiweze kufanya uchaguzi. Chama cha Mapinduzi kina vyanzo vyake vingine vingi na siyo pesa hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimwombe Mheshimiwa Dkt. Mpango kwa sababu wenzetu wanafikiri kwamba eti Azimio hili unalolileta la kufuta hizi bilioni eti ni pesa ambazo zitatumika kwenye uchaguzi, la hasha. Sasa nimwombe arudishe nyuma kidogo kwa sababu tumekuwa tukifanya jambo hili ili waone kwamba je, pesa tulizofuta hapo awali zilikuwa za uchaguzi?

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, niwaombe wenzangu wa Chama cha wenzetu kule akina Mheshimiwa Lema na wengine, si vizuri sana kuwa mnasingizia Chama cha Mapinduzi eti pesa hizi wanazichukua kwa ajili ya kazi hii. Tukianza kufanya hivyo hatuwezi kufika mbali, nina uhakika kabisa Ofisi ya Bunge inafanya kazi na Ofisi ya CAG na siku zote PAC na LAAC inafanya kazi na Ofisi ya CAG na siyo mara ya kwanza PAC kupewa taarifa kutoka kwa CAG na siyo mara ya kwanza Kamati ya LAAC kupewa taarifa za baada ya kukagua kwamba pesa hizi zinatakiwa zifanye hivi au kuna upungufu kwenye eneo fulani.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe sana tuwe na utaratibu wa kuiamini Ofisi ambayo tunafanya nayo kazi kama ilivyo kwa Ofisi ya CAG, LAAC lakini tukianza utaratibu wa kuanza kuhoji chombo ambacho tunafanya nacho kazi nafikiri tutakuwa tunawashusha morari wenzetu wa Ofisi ya CAG.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango nirudie, nimalizie kama atakuwa nafasi yake nzuri tu, hebu alete Maazimio ya nyuma ambayo tumeshawahi kuyafanyia kazi kwa kufuta kiasi cha pesa ambacho siku zote tumekuwa tukifanya hivyo, kwa sababu huu ndiyo utaratibu na tumekuwa tukifanya hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono Azimio lililoletwa na Waziri wa Fedha na nakushukuru sana. (Makofi)