Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya eneo la Pori la Akiba la Selous kuwa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya eneo la Pori la Akiba la Selous kuwa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Spika, kila Mtanzania atakubaliana nami kwamba Taifa hili kwa miaka mingi sana lilihitaji kuwa na Rais mwenye kufanya maamuzi, kutoa matamko ambayo kesho na kesho kutwa yatafanyiwa kazi na kuwa sheria. Kwa hiyo, sisi wananchi tunaotoka kwenye eneo la Pwani ya Kusini tunapendekeza sana Mheshimiwa Rais kwa kutoa tamko la kuamua sasa eneo hili la Selous kuwa ni Hifadhi ya Taifa ya Mwalimu Nyerere.

Mheshimiwa Spika, huu ni utaratibu mzuri kabisa wa kizalendo wa kuwaenzi wapigania uhuru akina Mwalimu Nyerere, lakini pia ninaamini huko tunakokwenda mbele katika eneo letu la Rufiji, basi kutapatikana eneo ambalo pengine tutaliita Bibi Titi Mohamed ambaye yeye alikuwa ni Mbunge wetu wa kwanza kule Rufiji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi wananchi wa Pwani ya Kusini tunaamini kabisa kwamba kwa miaka mingi sana tulipuuzwa na hili lilitokana na mgawanyo hafifu wa pato la Taifa na ilisababisha kuwepo kwa umasikini wa hali ya juu, lakini Watanzania na wananchi wote wa Tanzania pamoja na dunia nzima inatambua uwepo wa utajiri mkubwa sana katika eneo la Pwani ya Kusini. Kwa hiyo, sisi wananchi wa Rufiji tunampongeza sana Mheshimiwa Rais, lakini lazima nichukue fursa hii kuipongeza sana Wizara ya Maliasili na Utalii, Waziri wa Maliasili na Utalii anachapa kazi kweli kweli, kwa hiyo, sisi tunampongeza sana na maamuzi haya ni maamuzi sahihi, lakini tunatambua vipo vikwazo viwili pengine katika kuelekea uanzishwaji wa Hifadhi ya Taifa ya Mwalimu Nyerere yako mambo ambayo pengine ni lazima tuyazingiatie na tuyatekeleze sasa.

Mheshimiwa Spika, ikumbukwe kwamba miaka ya 2006 Serikali iliamua kuhamisha mifugo kutoka Hifadhi ya Bonde la Ihefu na kupeleka katika eneo la Kusini pamoja na Pwani kule Rufiji na kuendelea Kilwa na Mtwara. Tatizo la uwepo wa mifugo katika eneo la Hifadhi hii ya Mwalimu Nyerere litakuwa ni kikwazo kikubwa sana kwa kukua kwa eneo hili la hifadhi.

Mheshimiwa Spika, tuiombe Wizara sasa kufanya maamuzi magumu, maamuzi sahihi. Taifa hili lina eneo kubwa sana, Tanzania hatupaswi kugombana kati ya wakulima na wafugaji, lakini pia hata wafugaji wanapaswa kuwepo katika maeneo yaliyoidhinishwa na Serikali. Tuiombe Serikali kufanya maamuzi ya makusudi kabisa kuondoa mifugo kwenye eneo hili la Hifadhi ya Mwalimu Nyerere kuanzia Rufiji katika Kata za Mkongo, Ikwiriri na kuendelea; maeneo haya ni maeneo yote ambayo tunayategemea sasa baada ya kuanzishwa kwa Hifadhi hii ya Mwalimu Nyerere. Uwepo wa mifugo katika eneo letu kutaathiri hata uanzishwaji au ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme pale, Bwawa la mwalimu Nyerere.