Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

Hon. Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi nitumie muda huu kuweza kumpongeza Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Waziri wa Maliasili, Naibu wake, Katibu Mkuu pamoja na watumishi wa Wizara hii ya Maliasili na Utalii kwa kuja na mpango mzuri huu wa kuyapandisha hadhi mapori haya ya Ugalla na Kigosi ili kuweza kuunganisha pamoja na Azimio la jana la Mwalimu Nyerere National Park ambayo ilikuwa ni Pori la Akiba la Selous.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanda yetu ya Ziwa imekuwa ni sehemu ambayo kwa kweli ni chanzo cha uharibifu mkubwa wa mazingira hasa kwa wananchi wetu kuweza kuwa wakataji wa misitu na uharibifu wa mazingira kwa kiasi kikubwa. Kwa hiyo, hatua ya Serikali ya kuyapandisha mapori haya hadhi na kuyaita Hifadhi za Taifa ni hatua muhimu kwa maendeleo ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa maana hiyo mimi nitakuwa na mapendekezo tu machache juu ya jambo hili ya kwamba sasa kwa sababu tumeanza kuwa na national parks nyingi katika Kanda hii ya Ziwa, tukianza na zile za Burigi, Chato, Ibanda na Rumanyika na sasa tutakuwa na hii Hifadhi ya Kigosi pamoja na Ugalla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sasa Wizara pamoja na Serikali zianzishe Vyuo vya Utalii pamoja na Vyuo vya Misitu pamoja na Mamlaka za Manyamapori na vyuo mbalimbali vya kuweza kufundisha watu juu ya elimu ya utalii kwa sababu vitu hivi ni vitu vigeni katika maeneo haya na kwa maana hiyo wananchi wetu watahitaji kupata elimu zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije katika upande wa Azimio la Kuridhia Mkataba wa Minamata na matumizi ya zebaki. Mimi niseme tu kwamba kwa kweli jambo hili naliunga mkono kwa sababu sisi pia ni waathirika wa masuala haya ya matumizi ya zebaki kwa sababu ni wazalishaji wa dhahabu na tuna wachimbaji wadogo wadogo ambao wanatumia mambo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa maslahi ya muda, naomba kuunga mkono hoja, ahsante sana kwa kunipa muda. (Makofi)