Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jana tulipokuwa katika mafunzo ya watu wanaoshiriki katika Mabunge mbalimbali ya Afrika, tuliambiwa kwamba nchi yetu inachelewa kuridhia mikataba. Kwa mujibu wa viwango vya mikataba hii ambayo imeletwa leo hapa lakini specifically huu wa Marrakesh haujachelewa kabisa kulinganisha na mikataba mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkataba huu ni muhimu sana kwa sababu unakwenda kusaidia kundi kubwa la watu wetu. Maelezo yanasema kwamba watu wasioona, wenye uoni hafifu na ulemavu wa kusoma (print disabled) na hawa baadhi ni wale ambao kwa lugha ya kiingereza wanaitwa Dyslexia ambao wanaona sawasawa, wana intelligence sawasawa lakini ni slow leaners. Wale ambao kwenye shule tunasema mbona huyu haelewi, mbona huyu anachelewa kuelewa, nao wamekuwa considered katika mkataba huu. Kwa hivyo, mkataba huu unakwenda ku-cover kundi kubwa katika jamii ambalo hivi sasa linakosa fursa ambazo wangeweza kuzipata kwa kuwa mkataba huu umechelewa kuja kidunia lakini sasa hivi tayari upo na ndani ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo mengi ya kufanya kama nchi. Mojawapo ni kama ilivyosema hotuba ya Kambi ya Upinzani na hotuba ya Kamati kwamba kuna haja sasa kutengeneza sheria kwa haraka kuhusu copyright. Hilo liende sambamba na kuwaambia watu wetu wa ndani kwa mafunzo, maelezo na semina juu ya umuhimu wa kutengeneza kazi hizi na wao wajue kwamba kazi zao zinaweza kukuzwa ili watu kama hao waweze kuzitumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kingine ni namna ambavyo tunaweza kuwa na kanzi data ya uhakika ili wale ambao wanafaa kupewa hizo kazi ambazo zimekuzwa na siyo kutafsiriwa, kutafsiriwa haimo katika hili, ni kukuza maandishi ili waweze kuona basi kuwe na uhakika kwamba wanaopewa ni watu sahihi. Tunaomba pia taasisi ambayo itahusika na labda wengi wetu tunafikiri ni kama Chama cha Watu Wasiiona au Shirikisho la Watu Wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) ambao wao ni authorized kwa mujibu wa mkataba huu ili na wao waweze kutumia vizuri nafasi hiyo na wasiitumie vibaya kiasi kuweza kuathiri vibaya mkataba huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nafikiri kuna haja, kwa sababu tumechelewa kuingia katika mkataba huu ingawa siyo sana kama watu walivyosema kwamba zaidi ya nchi 70 zilishajiunga, ya kwenda kujifunza kwenye nchi nyingine wamefanya nini hadi hivi sasa. Moja ya nchi hiyo ni Australia ambayo iko mbele sana katika mkataba huu. Naishauri Serikali ikafanya utaratibu, sidhani kama Afrika tumekwenda mbele sana lakini kama ziko nchi zimekwenda mbele sana basi pia tujifunze kwenye nchi za Kiafrika nini wao wamefanya japokuwa tumechelewa kujiunga lakini tusifanye makosa yale tukafanya vizuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ni haja sasa ambapo tunasema mara kwa mara kutengeneza kanzi data. Kila siku tunaambiwa kuna kanzi data lakini jambo kama hili sasa unakuja umuhimu sana kuonesha kwamba ili tuweze kufanya makisio, ili hiyo kazi ichapishwe kwa haki ya kukuza vya kutosha ni muhimu kuwa na kanzi data juu ya watu wasioona, wenye uoni hafifu na wale ambao wana print disabled.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, ingawa katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri halikuwemo kuhusu suala la Marrakesh, ametuambia hapa kwamba Zanzibar imeshirikishwa lakini ingependeza katika Waraka huu rasmi wa Bunge na record zikaonesha kwamba Zanzibar ilishirikishwa. Hata hivyo, ukisoma Waraka huu hamna maandishi hayo kwamba Zanzibar ilishirikishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)