Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami naomba kuchangia na nitajikita zaidi kwenye hii Itifaki ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za SADC kuhusu Kulinda Hakimiliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ni kuhusu asilimia moja ya pato ghafi la Taifa kutopelekwa kwenye utafiti. Ni kwa muda mrefu sana Serikali yetu haipeleki asilimia moja ya pato ghafi la Taifa kwenye mambo ya utafiti na leo tunaenda kuridhia Itifaki hii, kama fedha hazitapelekwa tafsiri yake ni kwamba tunaenda kuwanufaisha wale ambao watakuwa tayari kupeleka fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kwamba nchi kama Afrika Kusini imeendelea sana na iko serious sana kwenye mambo ya utafiti, leo tunaenda kushindana nao hao kwenye suala hili lakini kwa sababu wao wako serious na sisi hatujawahi kupelekea fedha huko, Serikali ituambie baada ya kupitisha Itifaki hii watakuwa tayari sasa kuanza kupeleka fedha za utafiti ili tutakachopitisha leo hapa au tutaporidhia Itifaki hii isije mwisho wa siku tukashindwa kuwasaidia watafiti wetu. Kwa hiyo, nadhani hili ni jambo muhimu sana isije kuwa tunasindika wenzetu ambao tuko nao lakini wao wamejiandaa kuliko sisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni kuhusu fedha za maendeleo ambazo mara nyingi hapa Bungeni tumekuwa tukizipitisha au kuidhinisha lakini fedha hizi hazitolewi. Kwa mfano, leo tunapozungumzia suala hili la Hakimiliki za Wagunduzi wa aina mpya za mbegu maana yake hizi ni fedha za maendeleo na tunajua kwenye fedha za maendeleo Serikali hii ya Awamu ya Tano naona haijajipanga kabisa kwa sababu mara nyingi sana imekuwa ikisuasua kupeleka fedha kama Bunge linavyoidhinisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, mwaka 2016/ 2017, zile fedha za maendeleo zilizokuwa zimeidhinishwa na Bunge hili shilingi bilioni 100.527 zilipelekwa shilingi bilioni 2.2. Sasa kama zilipelekwa fedha hizo na hapa tunapitisha Itifaki hii, je, utekelezaji wa haya mambo inakuwaje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2017/2018 tulipeleka asilimia 11 tu ya fedha za maendeleo ambazo ziliidhinishwa na Bunge hili. Sasa leo tunapitisha Itifaki hii na kwenye Itifaki hapa tunaambiwa bajeti lazima itatumika, sasa inakuwaje kama hatutatenga fedha za maendeleo kwa ajili ya kwenda kutekeleza mambo haya ambayo tunaenda kuyapanga leo? Kwa hiyo, niseme tu kwamba kama Serikali haijajipanga kwenye mambo kama haya ni bora tukawa na subira ili mwisho wa siku tujipange vizuri na baadaye tuangalie namna ya kuweza kufanya lakini kama watatuhakikishia na Mheshimiwa Waziri yuko hapa kwamba fedha za maendeleo zitatolewa vizuri basi hii Itifaki itatekelezwa lakini kama hazitatolewa kama ambavyo miaka ya nyuma zimekuwa hazitolewi, nadhani tutaenda kugonga mwamba na hatutafanikiwa kwenye suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ni suala la mbegu za asili. Serikali ituambie wamepanga utaratibu gani kuweza kulinda mbegu za asili. Nafahamu kwamba nchi yetu tumekuwa na mbegu za asili nyingi sana na nyingine zimeanza kupotea polepole. Tulikuwa na mchele mzuri kule Kyela na zamani mnakumbuka ulikuwa unanukia, ule wa Kamsamba leo Serikali imejipangaje kutunza mbegu hizi maana zinaingia mbegu hizo mpya na za kwetu za asili zinapotea.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.