Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia hoja hii leo. Namshukuru Mwenyezi Mungu aliyenipa nguvu kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu na kuweza kutoa mchango wangu kwa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi. Naanza kwa kuunga mkono hoja, napongeza juhudi na kazi nzuri inayofanywa na Profesa Joyce Ndalichako na timu yake akiwemo Engineer Stella Manyanya, pamoja na timu nzima ya Wizara na wakati huo huo nampa pole Mheshimiwa Stella Manyanya kwa kuondokewa na mama yake mzazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wizara hii ya Elimu ina umuhimu wake kipekee, hapo hapo naunganisha na kutoa pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa kupitisha lile azimio la kupatia elimu bure kuanzia darasa la kwanza mpaka sekondari. Jambo hili lina maana sana, kwa sababu linatoa nafasi na fursa kwa wanyonge wengi kupata elimu kwa watoto wao. Wote tunajua umuhimu wa elimu, kwa hiyo zinahitajika juhudi zetu za pamoja kuunga mkono Wizara hii, ili vijana wetu wote wapate elimu stahiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa elimu mpaka sekondari, ni bure kwa hivyo ningependekeza kwamba kidato cha tano na cha sita, vilevile tufanye jitihada, ili iweze kuwa bure vilevile. Kwa kuwa pale kuna watoto wa wanyonge wengi, ambao wameweza kupita kuanzia kutoka kwenye shule za kata mpaka wakafika pale.
Kwa hiyo, Serikali ifanye vile inavyoweza katika kuongeza ukusanyaji wake wa kodi au mbinu nyingine inakojua itapata pesa ili vijana hawa wasije wakakwazwa. Kwa kuwa vijana wa chuo kikuu wanapata mkopo, na hawa nao wapate, kwa kuwa form five na sixndio chimbuko la wataalam wetu, naamini juhudi za ukusanyaji wa kodi zitatuwezesha kufika hapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara pia iangalie na ipitie ihakikishe kwamba angalau Wilaya zote zina shule za A-level za kutosha, kwa mfano Wilaya kubwa kama Rufiji ina shule moja tu yaA-level pale Mkongo na hii Wilaya ni kubwa kuliko Mkoa mzima wa Kilimanjaro, kwa hivyo Wizara ifanye ranking kuhakikisha kwamba Wilaya zote zina shule hizi la A-level.
kusimamia kujenga shule za sekondari za kata katika Kata zote, na maabara na madarasa. Hili jambo limefanikiwa kwa juhudi za wananchi na Serikali
pamoja.
Dhana ya elimu bure inapata mtikisiko kidogo, hii dhana imelenga kuondolea wazazi wanyonge, kuweza kuwasaidia vijana wao wapate elimu, maeneo mengi maabara zimesimama kujengwa, madarasa yamepungua kasi ya kujengwa, maeneo mengi wazazi wamepunguza kasi ya kujitolea kushiriki kwa kisingizio kwamba elimu ni ya bure, naomba sana tusiieleleze Serikali, tuendelee na spirit ile ile ya kuunga mkono jitihada za Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuendelee kusisitiza wananchi waendelee kuelimishwa umuhimu wa kutimiza wajibu wao, tunakiri kwamba katika jambo hili la elimu bure ziko changamoto, na hilo ni jambo la kawaida kwa sababu jambo lolote la maendeleo huwa linavikwazo vikwazo, lakini tutashinda na tutafika tunakokwendea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijazungumza zaidi kuhusu masuala ya shule hizi za kata, naomba kwa ruhusa yako nizungumzie kidogo kuhusiana na sheria. Naomba nitanabaishe kuhusiana na Sheria za Shule za Kata, Sheria ya Elimu Namba 25 kama ilivyorekebishwa mwaka 1978, kwa Sheria Namba 10 ya mwaka 1995, imeweka utaratibu wa Kikanuni wa kuanzishwa shule za sekondari na msingi, kwa utaratibu wa sasa, tuna shule za kata ina maana sheria hii haizungumzii shule za kata, kwa hivyo kunahitajika marekebisho ya sheria, kujumiuisha shule ya kata.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile sheria na kanuni inayounda bodi za shule, inatoa maelekezo ya uteuzi wa wajumbe wa bodi katika mkoa; kwa kuwa sasa tuna shule za kata, tunahitaji malekebisho ya Kanuni ili tuweze kutoa wajumbe hao wa bodi kutoka kwenye kata.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilijitahidi sana kuanzisha Sekondari karibu 3,500 za kata kama sikosei, sasa niiulize Serikali hii inashindwaje kujenga vituo vya VETAkwa kila Wilaya ili hawa vijana wetu ambao ni wengi wakapate elimu ya amali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali pia ina vitu ambavyo tunategemea vijana wetu wafanye. Lakini tulifuta somo la elimu na elimu ya kujitegemea, kwa mfano kila Ijumaa iliku wakati wa mchana watu wanakwenda kufanya mambo ya bustani, kama ilivyokuwa setup ya Mwalimu Nyerere wakati ule. Sasa vijana hawa wanapomaliza, wanaishia kwenda kucheza pool kwa sababu ile elimu ya bustani haipo, kwa mfano siku hizi kuna elimu ya bustani katika sehemu ndogo inaitwa permaculture ingeweza ikaanzishwa kwenye shule mbalimbali kule, watu wakajipatia mboga, viazi na vitu vidogo vidogo. Kwa hiyo lazima tuchanganue zaidi kutafuta, utaalamu na teknolojia sasa wa kuweza kuzalisha katika sehemu ndogo zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijamaliziwa muda wangu, basi niombe Wizara ya hii ilekebishe curriculum,ili tuweze kupata masomo ya kilimo na biashara, michezo, ufundi, katika ngazi zote na masomo haya yatiliwe mkazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lipo suala kubwa sana la kupata mimba wasichana, hili ni suala linaleta matatizo, linaleta unyonge, kwa sababu Wizara ifikirie na izingatie kwa kina kwa uharaka ikiwezekana kuwarudisha watoto hawa kwenye madarasa. Hatusemi hivyo kama tunawatia washawasha ili wakapate mimba laa! Ilamimba nyingine zinakuja ni kwa accident, nyingine ni kwa kubwakwa, kwa hivyo tufikirie, unapomuadhibu kijana huyu asiendelee kusoma, umemuadhibu na mtoto atakayezaliwa, umeiathiri familia yake nzima, umeongeza umaskini, hujauondoa umaskini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini uadhibu mtoto ambaye hana makosa, na yule ambaye mhusika mwingine mara nyingi anakwenda wanaposema wazungu anakwenda scot free, kwa sababu huwezi kumpata na hivyo anapata nafasi ya kwenda kufanya uharibifu, kuwawekea mimba watoto wengine.
Sasa tuone Wizara, sisi Wizara ya Elimu kule Zanzibar kwa mfano wameliona hili na wasichana wanaopata mimba kwa bahati mbaya, wanaendelea na masomo yao na imeonekana kwamba wengine hawa wanatokea kuwa wataalam wakubwa, wakatoa na mfano mzuri katika jamii, na mchango mzuri katika jamii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wizara yangu wakati nilipokuwa nahudumu kama Waziri, nilifika Bahamas. Nikatembelea darasa zima nikakuta watoto wote ambao wana miaka 16 hivi nakuendelea wote darasa zima wana mimba matumbo kiasi hiki. Lakini wameandaliwa darasa lao na wanafundishwa, kwa sababu huwezi kum-penalized huyu mtu, ile mimba inatokana na hali ya maumbile, saa nyingine huna nguvu za kumshinda mwanaume. Mimi baba yangu alisema usiende ukaa faragha na mwanaume itakuwa taabu.