Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE - WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama kwanza kabisa kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa michango yenu mizuri ambayo kusema ukweli imezidi kuongezea yale ambayo Mheshimiwa Rais aliyasema siku ya hotuba yake. Kwa hiyo, tumeendelea kupata mambo mengi zaidi ambayo yatatusaidia kuyafanyia kazi. Mmesema mengi katika sekta ya afya, kilimo, mambo ya utawala, utumishi, ukusanyaji wa mapato na mambo mengi sana mmeyasema ambayo yanaangukia katika Wizara yangu ya TAMISEMI.
Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kuwahakikishia kwamba yote haya tunayafahamu. Tanzania mpya ya Magufuli inayokuja, ni ya watu kufanya kazi. Tunataka tuwahakikishie kwamba Mheshimiwa Rais anaendelea kuisuka Serikali na mtambue kwamba Serikali bado haijakamilika. Bado tunahitaji Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, lakini tutakwenda mbali zaidi; tunataka kusuka vizuri sana Wakurugenzi mpaka Wakuu wa Idara. Tunataka tuwachuje, wawe na vetting nzuri kabisa na siyo kuokotana tu. Tunataka Tanzania mpya, tukisema kuanzia juu Hapa Kazi Tu basi ni Hapa Kazi Tu! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mengi yaliyosemwa hapa liko moja ambalo limejitokeza sana juu ya elimu bila malipo. Elimu bila malipo limesemwa na Wabunge wengi na ni kwa sababu halifahamiki. Serikali imeamua hata wakati bajeti haijafika, lakini kupitia kwenye wigo ule ule wa bajeti ya mwaka 2015/2016 kunyofoa katika utoaji wa huduma ya elimu, katika vote ya Wizara ya TAMISEMI kuhakikisha kwamba tunapata shilingi bilioni 131.88 kwa ajili ya kuanza kutoa elimu bila malipo kwa watoto wetu wa kuanzia chekechea hadi kidato cha nne. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kila mwezi tumepanga kupeleka shilingi bilioni 18.777 ambazo zimegawanyika katika maeneo manne. Kwanza ni fedha kwa ajili ya mitihani ya kidato cha nneambayo Serikali italipa moja kwa moja Baraza la Mitihani. Kwa hiyo, watoto wote kuanzia darasa la nne, form two, lakini kidato cha nnewenyewe watalipiwa na Serikali. Pili, ni fedha kwa ajili ya fidia ya ada, badala ya ile ada ya shilingi 20,000/= na shilingi 70,000/= Serikali inalipa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, fedha ya uendeshaji wa shule za msingi na sekondari, hizi zote Serikali italipa. Fedha kwa ajili ya chakula shilingi 1,500/= kwa kila mtoto wa shule maalum za msingi na kila mtoto wa shule za bweni za sekondari. Sasa kwa zile shule za bweni za sekondari, kwa zile shule za hostels ambazo zimejengwa na jamii hili limeleta mkanganganyiko kidogo, kwamba zile shule za bweni ambazo zimejengwa na jamii kupitia mipango yao wenyewe, kupitia wadau wengine wa maendeleo, hizi si hostels zinazotambulika na Serikali. Tunafahamu zipo, lakini siyo zile ambazo Serikali inapeleka fedha kwa ajili ya chakula. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tutambue kwamba shule hizo ni karibu shule 3,252 zenye watoto karibu 1,334,280, ni wengi sana. Kwa hiyo, huwezi ukakurupuka ukaja na mpango wa kuwalisha wale; tumeona tuanze na hawa wa bweni lakini baadaye kama itawezekana, tunaweza tukaenda huko, lakini siyo jambo ambalo sisi katika fungu hili la sasa, tumeliwekea.
Mheshimiwa Naibu Spika, nachukue nafasi hii kuwaomba wadau, wazazi na Halmashauri husika maana ndiyo wadau muhimu katika mamlaka zile. Kama zilianzisha shule hizi za bweni, basi zijue utaratibu ziliokuwa zinautumia, ziendelee nao, lakini utaratibu huo sasa usiwe unatoka katika maagizo ya Wakuu wa Shule kuwaagiza wazazi wawalazimishe kuhakikisha kwamba watoto wao wana chakula, wanaleta bwenini. Sisi tumesema hizi shule siyo za bweni ni za kutwa. Kwa hiyo, tunaamini mtoto atakaa nyumbani na atakuja kusoma shuleni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama kumekuwa kuna jitihada ya kuwafanya wakae shuleni, ni jitihada ya nyongeza tu na hivyo jukumu lile linabakia bado kwa utaratibu ule ule wa wazazi na wadau na pengine mamlaka zao zilizoamua ziwepo hizo shule, lakini siyo jukumu la Serikali kwa sasa mpaka hapo baadaye.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeona nielezee hili kama sehemu ya jambo lililoletwa mkanganyiko mkubwa. Ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)