Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Naomba kuchangia Wizara hii muhimu sana kama ambavyo Mheshimiwa Zitto alivyosema, inachangia kwa zaidi ya one third.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nianze kwa kuzungumza masuala ya TCU na niseme kwa kweli uamuzi huo wa kuivunja umechelewa kwa sababu ni kwa muda mrefu sana nimeongelea suala la vyuo hivyo pamoja na Kampala, japo sijajua Kampala inaendeleaje. TCU, kwanza niilaumu sana kwa jinsi ambavyo imekuwa ikidahili vijana ambao wanajua kabisa hawana uwezo. Nilikuwa nataka Serikali ituambie nini hatma ya vijana hawa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nalisema hilo kwa sababu kuna vijana 500 waliohamishwa kutoka kwenye Vyuo vya St. Joseph Songea na Arusha na hususani Arusha. Hapa nina barua ya TCU iliyoandikwa na Profesa Mgaya ikisema kwamba vijana wote waliokuwa kwenye vyuo hivyo, hii ikiwa ni pamoja na wale 500, watapelekwa kwenye vyuo vingine na vijana hao wamekwenda; na kifungu cha tano kinasema kwamba wanafunzi wote ambao ni wanufaika wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, mikopo yao itahamishiwa katika vyuo watakapokuwa wamehamishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa ninapozungumza, vijana hawa wamehamia SUA toka tarehe 28 mwezi wa Tatu wengine wamehamia UDOM toka tarehe 9 mwezi wa Nne na wengine wamehamia Mkwawa. Hapa ninapozungumza, vijana hao hawajapewa hata shilingi moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisemi kwamba wasichana wataathirika zaidi, lakini nazungumza kama mzazi. Watoto hawa kama kweli wamekaa miezi miwili plus hawajapata kitu chochote, tunategemea tunapa wanafunzi wa namna gani? Vilevile nalaumu sana vyuo hivyo, inawezekanaje Wakuu wa Vyuo hao hawawasiliani na Bodi ya Mikopo ili kujua kwamba hawa watoto wanaweza hata wakasababisha fujo katika vyuo hivyo kutokana na hali waliyonayo? Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri unapokuja utuambie nini hatima ya vijana hawa kutokana na huu mwongozo uliotolewa na TCU?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, naomba nizungumzie suala la Walimu, sitaenda kwa details kwa sababu kila mtu ameliongea. Ni wazi kwamba elimu bora lazima iletwe na Walimu lakini vilevile Walimu hao kinachofuatia ni vitabu na hasa vitabu vya kiada. Ni jambo la kusikitisha sana kuona kwamba ile change ya Rada ya shilingi bilioni 75 ambapo najua shilingi bilioni 55 zimeenda kwenye vitabu, lakini vitabu vilivyotengenezwa ni vitabu ambavyo haviwezi kabisa kusaidia watoto wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbatia ametoa mifano nami sina sababu ya kuendelea kutoa mifano, lakini kama mtoto wa Darasa la Kwanza, la Pili na la Tatu hawa ndio watoto ambao kile anachoambiwa ndiyo hicho hicho ataendelea kukiamini maisha yake yote. Sasa kama kitabu nilichonacho hapa kimepigwa chapa mara saba lakini bado kina makosa makubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kimepigwa chapa mara ya kwanza 2000, 2004, 2006, 2007, 2009 mpaka leo ni mara saba, lakini bado ina makosa lukuki. Unaposema namba nzima ni moja mpaka 99 ni makosa makubwa sana, lakini ukiangalia humu ndani ni aibu. Unamwambia vitu 11 lakini unasema ni 10, kwa hiyo, mtoto yule ataendelea kujua ni kumi kumbe ni 11. Huyu mtoto atajuaje kuhesabu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, haishii hapo tu, ndiyo sababu tunasema Wizara ya Elimu ina matatizo makubwa sana. Kwa kweli kwa kuwa Waziri Kivuli wa hii Wizara nimeelewa mambo makubwa mengi ya kipuuzi; inawezekanaje kitabu kitoe ithibati mwaka 2006, lakini kitabu kimepigwa chapa 2007, inawezekanaje? Unawezaje kutoa ithibati kabla ya kitabu? Kwa hiyo, haya ndiyo mambo tunayoyasema. Wizara ina matatizo makubwa sana. Hata ukiangalia hii Sera ya Elimu, ni matatizo makubwa, kwa sababu huwezi kusema mtaala au curriculum inafundishwa. Toka lini mtaala ukawa unafundishwa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa kweli tuna matatizo makubwa sana. Nami ninaamini hivi vitabu ambavyo vimepitishwa kote huko na kupata ithibati wakati vina matatizo maana yake ni kwamba wana makusudi kabisa ya kuua elimu ya Tanzania, kwa sababu vitabu ukitoka Mwalimu ndiyo kitabu. Kama vitabu vina matatizo, watoto wanapata nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo hili la elimu kwenye shule zetu za msingi na Vyuo Vikuu, kuna tatizo kubwa sana katika elimu ya juu. Sasa hivi kuna watu wenye Masters na Ph.D Dar es Salaam na maeneo mengi, kazi yao ni kusaidia wanafunzi kufanya thesis.
Kwa hiyo, unakuta mwananfunzi anamaliza masters lakini has nothing in the brain. Wanafanya plagiarism ya hali ya juu. Naomba kujua kwa Mheshimiwa Waziri na Serikali kwa ujumla, hivi huyu bwana anayeitwa Msema Kweli alipotoa hiki kitabu cha orodha ya Mafisadi sugu wa elimu ambao wengine ni Mawaziri, Wabunge nakadhalika, hivi Wizara ilichukua hatua gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunaona vitu vinatolewa hadharani halafu Wizara haichukui hatua, maana yake ni kwamba wanabariki watu waendelee kusoma bila kuingia darasani. Kwa hiyo, nataka Serikali ituambie, ni lini wanachukua hatua kwa watu ambao wanafanya masters na Ph.D? Yaani mtu anajiita Doctor, kumbe siyo Doctor, unaenda kwenye mikutano, aibu tupu! Haelewi chochote, hawezi language hawezi nini? Sisi wenyewe ndio tunaoharibu elimu yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye mfumo wa elimu. Mfumo wa elimu hapa Tanzania ninavyojua mimi kama Mwalimu unaanza nursery kwa mwaka mmoja au miwili, unaenda shule ya msingi miaka saba, unaenda ordinary level kwa maana ya Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne, halafu unaenda advance level Kidato cha Tano na cha Sita then tertiary level, miaka mitatu mpaka mitano kutegemeana na na degree.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huo ndiyo mfumo wetu wa elimu. Kinachonishangaza leo na Mheshimiwa Waziri aje atuambie, ni lini mfumo huu umebadilika kwamba mwanafunzi anamaliza Kidato cha Nne moja kwa moja anaenda Chuo Kikuu? Imeanza lini na kwa utaratibu upi? Kwa hiyo, nataka tuelezwe sasa mfumo wetu wa elimu nionavyo sasa hivi, tumeamua kwamba kutakuwa na elimu msingi ya Darasa la Kwanza mpaka Kidato cha Nne. Nataka kujua tu, kwa nini tuna wanafunzi wanaomaliza Kidato cha Nne wanaenda moja kwa moja Chuo Kikuu kwa ajili ya degree? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nataka kuzungumza ni suala la utafiti wamezungumza wengi lakini niseme kwamba tulishafikiria na kuamua kwamba angalau utafiti upewe one percent ya GDP ya pato ghafi. Kwa takwimu za pato ghafi la mwaka 2013/2014 ilikuwa ni shilingi trilioni 44, naambiwa sasa hivi limeongezeka sana kama shilingi trilioni 90. Kwa hiyo, niliamini kwamba utafiti na hapa nazungumzia COSTECH ambao ndiyo wana mwamvuli wa tafiti zote. Kwamba wangepata sawa na shilingi bilioni 440 kwa pato la Taifa la shilingi trilioni 44.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hawa wamepata ten billion sawa na 0.025 ya pato la Taifa. Sasa hawa watu watafanyaje utafiti kama hawapati fedha? Mbaya zaidi, vyuo vyetu vikuu; Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa takriban miaka mitatu mfululizo hawajapata fedha za utafiti. Tunategemea kweli nchi hii itaendelea kuwa ya viwanda kama haiwekezi kwenye utafiti? (Makofi)
Mheshimiwa Mweyekiti, kwa hiyo nilikuwa nadhani tuna…
Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa
Mzungumzaji)