Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa hotuba yake nzuri; na uzuri huu unajionesha pia kutokana na michango ya Waheshimiwa Wabunge na wananchi ambao sio Wabunge. Tunasoma kwenye magazeti, tunaona kila mtu amefurahia hotuba yake, lakini hata utendaji wa wa awali kabisa ya Serikali yake ya Awamu ya Tano. Kwa hiyo, nampongeza sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, nawashukuru sana wananchi wa Jimbo la Ismani kwa kunirudisha tena hapa Bungeni. Nataka kuwaahidi tu kwamba kama nilivyozoea nitawatumikia na nadhani bado wana imani na mimi nitaendelea na nafasi yangu ile ile. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi niliyopewa na Mheshimiwa Rais ni kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Nataka kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba nimewasikiliza sana, yote yaliyosemwa mkifungua ukurasa wa 41 mpaka 46 mmezungumza katika maeneo hayo. Maeneo yote mliozungumza yako kwenye ilani, nataka kuwaahidi kwa sababu muda hautoshi, kwamba tunawawekea utaratibu wa kuyatekeleza katika miaka mitano hii. Kwa sababu tuko pamoja tumeshaunda na Kamati tutashirikiana katika kuhakikisha kwamba yote yaliyopangwa katika Ilani ya Uchaguzi wa Chama chetu yanatekelezwa katika kipindi hiki cha miaka mitano kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, yako mambo ya muda mfupi ambayo tumeamua kuyafanya na juzi mliniuliza. Moja kubwa mmezungumza ni habari ya migogoro, hili ni jambo la muda mfupi, liko kwenye ilani lakini halitaji miaka mitano. Tumekubaliana na rafiki yangu hapa kwamba mtuandikie migogoro; najua kuna migogoro ya mipaka ya vijiji kama nilivyosema, mipaka kati ya vijiji na hifadhi mbalimbali za misitu, wanyama na nini, mipaka kati ya Wilaya na Mikoa. Tukishapata hiyo orodha tutapanga utaratibu. Yale yanayohusu Wizara yangu na Wizara ya Maliasili tutaunda timu ya pamoja na bila kumsahau mwenzetu mwenye ardhi, Serikali za Mitaa ili kuhakikisa kwamba tunapitia migogoro yote na kuipatia majibu. Kwa hiyo, ni jambo ambalo tutaanza nalo sasa, haliitaji bajeti kubwa, ni lazima tuondoe hii migogoro kwa sababu imedumu na imewatesa sana wananchi, hilo tutalifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Wizara yangu sasa hivi tunafanya audit ya ardhi. Wako watu tuliyowapa mashamba makubwa lakini hawayatumii vizuri, vilevile wapo watu tumewapa mashamba makubwa, wameweka rehani na bahati nzuri mtu yeyote akiweka rehani mortgage, mimi najua kwa sababu lazima mortgage zile zinasajiliwa kwangu. Wameweka matirilioni za fedha lakini tunataka kujua kwenye mashamba yao hizo trilioni za fedha wameweka?
Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya mashamba ambayo nimeshayapitia nimegundua pamoja na mamilioni ya fedha waliyochukua, mashamba yao yako vilevile kama walivyoyachukua. Kwa hiyo, tunataka tujue hizi fedha wamepeleka wapi? Kwa hiyo, tunafanya audit kwa watu waliochukua mashamba makubwa kwa maana ya kwamba kama wameshindwa, sheria iko wazi, tutawanyang‟anya, tutawapa wananchi wenye shida au tuawapa wawekezaji wengine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tunataka tujue, wale walio mortgage fedha hizo wamepeleka wapi? Kwa sababu sasa iko tabia ya watu kuchua mashamba makubwa sana, tena watu wa aina fulani tu, wanachukua mashamba kila mahali, lakini hawawekezi, wala hawayatumii. Sasa wanachukua kama rehani ili wapate pesa, waende kujenga magorofa kigamboni kwa Mheshimiwa Ndugulile. Hiyo hatutakubali. Tunataka ukichukua fedha, lazima uwekeze katika mashamba yale yale.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hizi ni hatua za muda mfupi, kuondoa kero ya migogoro ya ardhi inayosababishwa na mipaka ambayo sisi watu wa Serikali tunaweza kufanya; lakini ya muda mrefu iko kwenye ilani. Lengo la Serikali katika Ilani ya Miaka Mitano ni kupima kila kipande cha ardhi. Tunaanza mpango huu mwezi ujao kwa Wilaya mbili ya Kilombero na Ulanga. Tunapima kila pande cha ardhi, lazima kiwe na mwenyewe na kumilikishwa kwa hati. Tunafanya Wilaya mbili za majaribio, Ulanga na Kilombero tunaanza mwezi ujao.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu tungependa hatua kwa hatua ardhi yote ya Tanzania ipimwe na ikipendeza zaidi, kila mwananchi awe na fursa ya kumiliki ardhi yake kwa hati ili aweze kuitunza, lakini na Serikali iweze kupata mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, yako malengo ya muda mrefu. Nilitaka tu niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge mliosema mengi, tutatembea sana, tutawakuta huko huko, lakini nataka muwahakikishie wananchi kwamba ile migogoro mikubwa ambayo imewakera kwa muda mrefu, tutaisimamia.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)