Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nami kunipa nafasi. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, wote wanawake. Tunategemea kuona ni jinsi gani wanawake mnaweza na sisi tuko nyuma yenu, tutawaunga mkono, tuna imani mtafanya vizuri ninyi akina mama ni walezi. Mungu atawasaidia katika kazi yenu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile ni dakika tano, naomba niende moja kwa moja. Mimi kwa vile ni Mbunge ambaye natoka Mkoa wa Dar es Salaam wenye utitiri wa shule za private, nitakuwa mkosefu wa fadhila au nitakuwa mnafiki iwapo sitazungumzia suala la ada elekezi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kabisa mchango wa sekta binafsi katika maeneo mbalimbali ya maendeleo hususan katika suala zima la elimu. Natambua jinsi gani shule za binafsi zinatubeba kama Mkoa wa Dar es Salaam na kuweza kupata matokeo mazuri. Pia ni wajibu wangu kusema changamoto ambazo wananchi wangu wanazisema kila siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ada za Shule ya Msingi na Sekondari, mpaka sasa imeambukiza na Vyuo Vikuu, ni tatizo. Ada hizi zinapanda kila baada ya muda. Wazazi hao hao ndio wanaokuja kwangu mimi kama Mbunge. Wengine wanashindwa, wanaomba niwasaidie kuwapeleka Olympio. Olympio shule ni moja Mkoa mzima wa Dar es Salaam, ndiyo shule ya Serikali; Olympio na Diamond. Sasa hawa watoto ambao wanashindwa huku, tutawapeleka wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wale wengine wanapata matatizo wazazi wao hali ya uchumi inakuwa mbaya, wanashindwa kuendelea na shule. Pia kumpeleka mtoto wako shule ya private mara nyingine siyo wingi wa kipato ulichokuwanacho, ila ni utashi wa kupata elimu.
Kwa hiyo, naomba waelewe hata wenzetu, kwamba tunapokwenda kule, siyo kwamba mimi nina hela nyingi. Vijana wetu ambao ni watoto wetu ambao na wao wana watoto wenzao, wanakwenda kule wanakwama. Nao ndio wanaorudisha huku kwamba jamani hizi ada zenu zinazidi. Mtoto wa chekechea shilingi 3,800,000/=; hivi inakuaje? Ndiyo tunajua huduma anayoipata na nini, lakini tuangalie angalau kidogo. Vijana wangu mimi wa Clouds kila siku ndiyo maneno yao, wanasubiri Serikali, ada elekezi, leo mimi Mbunge wao nisimame hapa nisipolizungumzia, kwa kweli sitawatendea haki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za binafsi hazikuanza leo wala jana, kwanini wananchi walilipokea? Tena walipoke vizuri. Leo kila mtu anazungumzia suala la ada; hapa kuna jambo. Naiomba kabisa Serikali, ikae na hao wenye shule tuangalie jinsi gani ya kuweka utaratibu mzuri ili shule zetu ziwe angalau na udhibiti wa aina yake. Shule ya Msingi au Sekondari inafika mpaka shilingi milioni tisa. Hivi leo shule ya shilingi milioni tisa, mtoto yule anaenda; baba yake kafariki, ukienda hawampokei. Wanakushauri ufanye nini, ufanye nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tusema ukweli, pamoja na utoaji wa huduma, lakini na biashara ipo. Kwa hiyo, naiomba kabisa Serikali; kama isingekuwa biashara, isingetofautiana bei. Sasa inakuwa elimu kama inauzwa; hapa unaona shilingi 200/=, hapa shilingi 300/= au shilingi 3,000/=. Siyo sawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tena, pamoja na mambo yote, tuna shule za private, yaani English Medium Dar es Salaam mbili; Olympio na Diamond. Hivi Serikali lini italiona hili suala? Kama wananchi sasa hivi wamekuwa wanapenda watoto wao wasome English Medium kwanini zisiwekwe katika Wilaya ya Temeke, Kinondoni, lakini na mikoa mingine pia ili wale watoto ambao watakwenda huko wakipata matatizo, warudie kwenye shule hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie TCU. TCU Mheshimiwa ni matatizo! Hivi leo udahili wa wanafunzi, mimi mtu mzima nataka kusoma Chuo, naambiwa niende TCU sijui nikapeleke matakataka gani, vitu kibao! Hivi mambo mengine si wanajichanganya wenyewe! Utakuta mkopo unakuja kwangu, mimi nautaka? Hii yote inakwenda na mfumo mbaya. Wanatakiwa wabadilike, warudishe mambo mengine kwenye kwenye Vyuo Vikuu vyenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyuoni tumeweka Uongozi, tunawaamini…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)