Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nichangie angalau kwa dakika tano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Waziri mwenye dhamana, Naibu Waziri, Watendaji wote wa Wizara hii ya Elimu, wanafanya kazi nzuri, mwelekeo tumeshauona nadhani tumeuanza vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la Walimu wa Sayansi ambao Wabunge wenzangu wamelizungumzia sana. Sasa tatizo ambalo naliona, bila kuona namna gani tutalitaua, tutaendelea kuwa na tatizo na Walimu hawa wa Sayansi. Kwa mfano, Walimu hawa kila mwaka wanaopatikana ni wachache; na tatizo kubwa ambalo linajitokeza ni kwamba baadhi ya sisi wazazi; Walimu wenyewe tunawajengea mazingira watoto kwamba somo hili ni gumu. Hili ndiyo tatizo! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hebu tuone namna gani tunaanza kujenga misingi huku chini kutoka Shule za Msingi mpaka Sekondari kuona watoto wanapenda somo hili. Tukitengeneza vizuri watoto walipende somo hili, tutamaliza tatizo la Walimu wa Sayansi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzangu wamezungumzia suala la shule binafsi. Shule za watu binafsi, naweza kusema ni sawa na hospitali za watu binafsi ambazo zinahudumia na Serikali inapeleka ruzuku pale. Hata Mwalimu Nyerere wakati ameanza kuambia Taasisi mbalimbali… (Makofi)
MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hata Mwalimu Nyerere wakati anaanzisha shule za watu binafsi, Taasisi za kidini na kadhalika, ilikuwa ni kuisaidia Serikali. Kwa hiyo, nadhani sasa muda umefika, tuone namna ya kusaidia shule hizi kwa sababu na zenyewe zinatoa huduma. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi Shule za Sekondari ambazo tumezianzisha katika Kata mbalimbali, Serikali imefanya kazi nzuri; tusimamie, ziboreshwe zilingane na hizi na baadaye hizi zitajifuta pole pole zenyewe. Hii ya kuelekeza kwamba kuwe na ada elekezi, sioni kama tutakuwa tunafanya kazi vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo linguine ni suala la Walimu. Kwenye Halmashauri yangu ya Mji wa Makambako, nilikuwa nadhani TAMISEMI Wizara hii ya Elimu, hebu tuone namna hii ya kuhakiki madeni haya haraka ili Waalimu hawa waweze kupewa stahiki zao. Wenzangu wengi wamesema hapa, Walimu wanafanya kazi nzuri sana; sasa tuone namna ya kuhakiki madeni haya ili waweze kulipwa stahiki zao haraka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo haya, nirudie tena, shule za watu binafsi zinafanya kazi nzuri, Serikali, isaidie kabisa. Zinafanya kazi nzuri sana. Tuwatie moyo! Mwaka 2015 shule hizi za watu binafsi zimefanya kazi vizuri, zimetoa watoto waliofaulu sayansi vizuri. Sasa kwanini tusiziunge mkono? Kwa nini tusiwasaidie?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii ya Waziri wa Elimu asilimia mia moja kwa mia moja, baada ya kuona haya marekebisho ya ada elekezi yaondolewe. Nakushukuru sana.