Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema mwenye kurehemu. Pia nampongeza Mheshimiwa Spika, yeye binafsi kwa kuwa makini sana kusimamia Bunge hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia katika meneo yafuatayo: maslahi duni ya Walimu, kubadilisha syllabus pasi kushauriana na Wizara ya Elimu Zanzibar; NECTA; kutolipatia stahiki somo la dini ya Kiislam mashuleni kuhusiana na ufaulu wa wanafunzi; shule za binafsi; mikopo ya elimu ya juu; kufuta mfumo wa GPA na kurejesha divisions; na elimu bure.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na maslahi duni ya Walimu. Hapa ndipo hasa penye matatizo makubwa sana katika kada ya elimu. Walimu wanalipwa mishahara duni. Hii inapelekea sana Walimu kufanya kazi bila ya utulivu kwa sababu umasikini ni mwingi, wanashindwa hata kujikimu. Ingekuwa vyema maslahi ya Walimu yakaangaliwa upya. Mwalimu wa Tanzania amekuwa kama mshumaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kubadilisha syllabus bila kushauriana na kupeana taarifa kwa wakati stahiki inasumbua sana. Wizara ya Elimu Zanzibar haishirikishwi wakati wa kubadilisha syllabus hasa kwa madarasa ya Kidato cha Kwanza hadi cha Nne.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nizungumzie chombo cha NECTA. Naomba nipatiwe majibu, Zanzibar inashiriki vipi katika chombo hiki? Ni vyema pangejengwa Ofisi ndogo basi ya NECTA kule Zanzibar ili kuzuia kwenda Dar es Salaam kila siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu ambao wanachaguliwa kusimamia mitihani ya CSEE wengi wao hawana sifa na kwamba masharti yanayotakiwa hayazingatiwi. Hii hupelekea kuwepo na matatizo mengi sana wakati wa kufanya mitihani hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ubadilishaji wa mitihani (matokeo) kutoka GPA kwenda Division ni vyema ukaangaliwa tena kwa utafiti wa kina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende sasa kwenye shule binafsi. Shule ni nzuri na mimi binafsi ninakubaliana nazo sana. Ila ni vyema Serikali nayo ikazifanye shule zake ziwe na uwezo angalau kama hizi. Maabara za shule za Serikali ni vituko! Walimu wazuri wote wamepotelea katika shule za binafsi, matokeo mazuri yako ndani ya shule binafsi. Kuna nini hapo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, inasadikika kwamba somo la dini halipatiwi stahiki zake katika ufaulu wa kuendelea Kidato cha Tano. Naomba hapa nipatiwe jibu, ni kweli au la? Kama ni kweli, ni kwanini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mikopo ya wanafunzi wa Vyuo Vikuu ni vipi Zanzibar inapatiwa gawio lake na kwa wakati upi? Pia dhana ya elimu bure haijaeleweka ipasavyo? Ni vyema ikaelezwa vizuri sana na ikaonekana kiutendaji, naomba kuwasilisha