Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kwa maandishi katika Wizara hii. Kwanza nianze na suala la wabunifu wa teknolojia katika nchi hii. Nchi hii wapo watu ambao wana ubunifu wa kutumia teknolojia, lakini hawajulikani wala kutambulika na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano wa Kampuni ya Young Scientist Tanzania ambayo huwasaidia kuwaendeleza vijana chipukizi wa ubunifu na teknolojia, Kampuni hii mwaka huu imewapa tuzo vijana wawili wa Shule ya Sekondari Morogoro ambao ni Edmund na John Method. Pia vijana hao Kampuni imewapelekea kusoma Dublin University huko Ireland kwa ajili ya kuendeleza vipaji vyao vya ubunifu na ufumbuzi wa teknolojia. Nashauri Serikali iwe inafuatilia vijana wabunifu kama hawa ili wanapomaliza masomo yao, Serikali iwashawishi kurudi nchini ili kutumia ujuzi wao kusaidia maendeleo ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kuboresha mishahara ya Walimu pamoja na mazingira ya kufanyia kazi kama vile nyumba, umeme na maji. Hii itaondoa upungufu wa Walimu mashuleni hususan shule za pembezoni mwa Miji. Walimu wengi wanapopelekwa au kupangiwa na Serikali shule za vijijini huwa hawaendi kutokana na mazingira magumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inahitaji kuongeza juhudi katika kutoa elimu bora ili kushindana na nchi nyingine duniani. Nasema hivi kwani wanafunzi wengi humaliza Kidato cha Nne ambayo ni elimu ya awali bila kujua kusoma na kuandika vizuri, lakini pia hata kutokuwa na uwezo na kujieleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha, naunga mkono hoja.