Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, VETA Wilaya ya Rungwe; Katika Wilaya ya Rungwe hatuna chuo cha ufundi na hii inatupa shida sana katika kuwaendeleza vijana wetu waliomaliza Darasa la Saba na Kidato cha Nne. Rungwe ni Wilaya yenye kutegemea kilimo sana hivyo uanzishwaji wa VETA kutasaidia vijana kujifunza elimu ya usindikaji wa mazao, ufundi wa kutumia mzao kama mahindi, migomba majani yake na kuwezesha kupatikana ajira kwa vijana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mabweni Wilaya ya Rungwe, upatikanaji wa mimba za utotoni ni shida sana katika Kata za Kyimo Masukuru. Je, Wizara haioni umuhimu wa kuwezesha Halmashauri ziweze kujenga mabweni ili kupunguza vishawishi, ulinzi kwa watoto wa Kata hizi. Nashauri Mkoa mpya wa Songwe upatiwe umuhimu wa kuanzisha vyuo, vikiwemo vya ufundi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Chuo cha Ualimu Mpuguso. Majengo ni chakavu kabisa idadi ya wanafunzi mabwenini siyo nzuri, miundombinu haifai, vitabu havitoshi kabisa. Pia shule ya sekondari Ndembela, Halmashauri imekuwa na deni la shule ya sekondari Ndembela takribani milioni 700 toka kanisa la Adventista Wasabato barua ya maelezo ya msaada ipo katika Wizara ya Elimu mimi nakumbusha Wizara ione umuhimu wa kulipa deni hilo na kuweka commitment kulibeba deni hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, posho na nauli za walimu. Walimu wamekuwa na madeni mengi sana Serikalini, pesa zao za likizo na nauli wafanyapo kazi nje ya kituo wengi wamekopwa na Serikali kwa muda mrefu sana. Kupandishwa madaraja pia imekuwa tatizo kwa walimu kukaa muda mrefu sana na pesa zao za uhamisho pindi wakipata uhamisho posho hizi zilipwe haraka.