Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Nafasi ya Makamu Mkuu wa Chuo ni muhimu sana katika maendeleo ya Chuo Kikuu chochote. Kwa muda mrefu Chuo Kikuu Mzumbe kinaendeshwa na kusimamiwa na Kaimu Makamu Mkuu (Acting Vice Chancellor), ninaomba Wizara iharakishe na ikamilishe taratibu za kupata Vice Chancellor wa Chuo Kikuu Mzumbe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna uhaba wa walimu wa awali kwa walimu wa awali ambao wamehitimu katika vyuo mbalimbali na wamekuwa wakijitolea kufundisha kwa muda mrefu ingekuwa vizuri waajiriwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya China ilibainishwa nia yake ya kushirikiana na Serikali yetu kujenga chuo cha Veta Mkoa wa Kagera. Naomba Wizara iongeze msukumo ili chuo cha VETA – Kagera kianze kujengwa. Eneo la kujega chuo hicho lipo na Balozi wa China Tanzania alishatembelea eneo hilo. Ninaomba pia Mheshimiwa Waziri akipata nafasi atembelee eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna walimu wengi ambao wanapandishwa madaraja lakini mishahara yao haibadilishwi, naomba Wizara ijitahidi kuhakikisha walimu wote wanalipwa stahili zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna utaratibu wa kufundisha unaitwa Montessori utaratibu huu ni mzuri na una manufaa mengi ukilinganisha na utaratibu wa kawaida tunaotumia. Aidha, hapa Tanzania kuna vyuo vinavyofundisha kwa kutumia mfumo huu. Ninaomba walimu waliofundishwa kutumia mfumo wa Montessori waajiriwe na Seikali. Aidha, kwa kuanzia, madarasa ya awali yanaanza kutumia mfumo wa Montessori kufundisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.