Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa dakika chache hizi za kuchangia na mimi katika hotuba ya Rais ya kufunga Bunge na hotuba ya kufungua Bunge la Kumi na Mbili.

Mheshimiwa Spika, kila mara ninapomkumbuka Dkt. John Pombe Magufuli na hotuba zake na uongozi wake inanikumbusha kitabu kimoja kilichoandikwa na Dkt. John C. Maxwell. Kwenye kitabu chake anasema; ikitokea vita kati ya kundi hili na kundi lile au kati ya nchi hii na nchi ile na ikatokea kwamba jeshi moja wanajeshi wake wote ni simba na kiongozi wake ni simba na jeshi lingine wanajeshi wake wote ni kondoo na kiongozi wake ni simba, basi hizi timu mbili zikipigana kwa maana ya timu ambayo kiongozi ni simba na askari ni simba na timu ambayo kiongozi ni kondoo na askari ni simba, definitely timu ambayo kiongozi ni kondoo itapoteza vibaya sana. (Makofi)

Lakini pia Maxwell akasema kwamba; pamoja na kwamba jeshi linaweza kuwa na masimba wote ilimradi tu kiongozi ni kondoo, lazima jeshi hilo litapoteza; alikuwa anaongea kwa habari ya dhana ya uongozi, kwamba maendeleo au ushindi ni kiongozi. Kwa bahati nzuri Tanzania tumepata kiongozi Simba na majeshi nayo ni simba na kwa hakika ushindi wetu upo kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini ninapokumbuka dhana ya uongozi wa kidiplomasia, ninakumbuka mambo mawili; kwenye diplomasia, uchumi wa kidiplomasia tuna mambo mawili; tuna uchumi pamoja na biashara, lakini kwenye diplomasia ya uongozi tuna mambo matatu; cha kwanza tunasema strong power, cha pili soft power na cha tatu smart power.

Mheshimiwa Spika, sasa strong power ni nini; strong power ni mahali ambapo kiongozi anashawishika kwamba watu wangu nikiwapeleka mpaka pale wantanufaika na maisha yao na maisha yao yatakuwa salama. Lakini watu wale ama kwa kujua au kwa kutokujua hawajui kwamba wakifika pale watakuwa salama. Sasa strong power maana yake ni kiongozi huyu anawakokota hawa watu wapende wasipende wakifika pale wakagundua faida zake wanamshukuru yule kiongozi wanasema ahsante kwa kutufikisha hapa, hiyo inaitwa strong power.

Mheshimiwa Spika, soft power ni kwamba unaanza kuwabembelezabembeleza, unawaeleza faida za wanakokwenda, watakakofika na mambo ambayo watayapata, unawabembelezabembeleza mpaka unawafikisha pale baadaye wanakushukuru wanasema ahsante kwa kutufikisha hapa, hiyo inaitwa soft power.

Mheshimiwa Spika, lakini smart power unaunganisha strong power pamoja na soft power; kuna wakati mwingine unawaburuza wanakwenda, kuna wakati mwingine unawabembeleza na hiyo ndiyo aina ya uongozi ambayo Dkt. John Pombe Magufuli anayo. Dkt. John Pombe Magufuli ni smart power na Mawaziri wetu na Waziri Mkuu pia ni smart power, watatufikisha tunakotakiwa kwenda kwa uhakika kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, TARURA; hai-make sense ukiona kwamba mtandao wa barabara za TARURA ni takribani kilometa 130,000 na mtandao wa barabara za TANROADS ni takribani kilometa 40,000, hai-make sense kwa nini mpaka leo TARURA anapewa asilimia 30 na TANROADS anapewa asilimia 70; hai-make sense. (Makofi)

Nikisema hivyo sina maana kwamba nadharau ukweli wa kwamba ubora wa barabara za TANROADS unatakiwa kuwa imara zaidi kwa sababu una-cut accross mikoa kwa mikoa, lakini hai-make sense kwa nini huyu ambaye ana mtandao wa kilometa 130,000 apewe asilimia 30 na huyu mwenye mtandao wa kilometa 40,000 apewe mgao wa asilimia 70; hakuna mateso tuliyonayo Wabunge kama TARURA kukosa fedha kule mikoani, ni ngumu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitoe mfano kwenye Jimbo langu la Kawe. Kwenye Jimbo la Kawe Wilaya nzima ya Kinondoni tuna kilometa za barabara za ndani 1,663. Kilometa 200 ziko Jimbo la Kinondoni kwa pacha wangu Mheshimiwa Tarimba, lakini kilometa 1,463 ziko Jimbo la Kawe; kilometa I,463, ni sawasawa na kutoka Dar es Salaam mpaka Kigoma lakini zote ziko ndani ya Jimbo la Kawe. Nilipowatembelea TARURA wana fedha za kutengeneza kilometa 120. Ina maana kuna kilometa 1,300 ambazo haziwezi kutengenezwa, this is not acceptable kwa wakati wowote katika nchi yetu; haikubaliki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na kama kweli tuna ndoto ya kuwaletea watu maendeleo, siyo Jimbo la Kawe tu, lakini kwenye kila jimbo barabara zinazotakiwa kujengwa kwa kutumia fund ya TARURA hazitajengwa kabisa kama TARURA hataongezewa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Road Fund kama unavyojua ni mawazo yaliyoanza mwaka 1999 mpaka 2000 nyakati zile Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa Waziri wa Ujenzi. Kuanza kuchukua shilingi 200 kwenye kila lita moja ya mafuta na kuchukua asilimia 70 kwenda TANROADS na asilimia 30 kwenda TARURA.

Ninawaomba watendaji wawaze mawazo mengine tena ya kuongezea fedha. wasitegemee mawazo yaleyale ya Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa Waziri wa Ujenzi, wawaze mawazo mengine ya kuongezea fedha. There is nobody here who is a copy of the other, everybody is an original from the Almighty God; lazima watendaji kazi wetu mjiongezee zaidi, muwaze zaidi, muwe creative zaidi kwa namna ya kumuongezea TARURA fedha, vinginevyo it is a nightmare kuwapa watu maendeleo kwa kupitia TARURA. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna huyu mdudu anaitwa Corona…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana, dakika tano zimekwisha. (Makofi/Kicheko)

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)