Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, muundo wa sasa wa kushughulikia masuala ya elimu nchini unaofanywa na Wizara mbili (TAMISEMI, na Wizara ya Elimu) umeleta mkanganyiko mkubwa sana. Elimu yetu siku za nyuma ilisimamiwa na Wizara moja na ndiyo maana tulifanya vizuri. Ninashauri Serikali kurudisha mfumo na muundo wa awali wa Wizara moja tu kama kweli tunataka kupiga hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao uhaba mkubwa sana wa walimu wa sayansi kwenye shule zetu hasa za sekondari za Kata. Mwalimu ana nafasi kubwa katika kumsomesha mtoto. Iweje mtoto anaanza form one hadi form four hajapatwa kufundishwa na mwalimu wa sayansi kisha watoto hao tunawapa mtihani baada ya miaka minne.
Ninashauri Serikali kufanya jitihada za maksudi kuhakikisha walimu wanapatikana. Serikali pia itoe motisha ya mishahara mizuri kwa walimu ili walimu wakae kwenye kazi yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za sekondari za Kata, mfano; Endallah, Endabash, Baray, Mangola, Upper Kitete, Kansay, Orbochand, Getamock zina walimu pungufu sana wa masomo ya sayansi. Ninaiomba Wizara ipeleke walimu hao Karatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ada elekezi huu siyo muda wake. Serikali iboreshe shule zake badala ya kutaka kupunguza ada kwa shule binafsi. Niulize, hivi humu ndani ya Bunge nani ana mtoto wake katika hizi shule za Kata? Tumepeleka watoto shule za binafsi baada ya kuona elimu inayotolewa huko ni bora kuliko ile inayotolewa katika shule za Serikali. Serikali iachane na ada hizo na kama kuna wazazi wanaona hizo shule za binafsi ni ghali basi wapeleke watoto wao kwenye shule ambazo ada zake wanazimudu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho Halmashauri ya Wilaya ya Karatu ilitoa majengo na maeneo yake Ayalabe karibu na Mji wa Karatu ili kuanzisha chuo cha Ualimu, miundombinu ya chuo hicho iko tayari. Nimwombe Waziri wa Elimu afike, akague chuo hicho ili kianze kutumika.