Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi nami niweze kuchangia mada iliyokuwa mbele yetu. Naomba niwakumbushe waumini wa makanisa 142 ya Gwajima, lakini pia waumini wa Tanzania juu ya Biblia inasema nini? Biblia inasema, katika Marko 16:18a, “hata tukila vitu vya kufisha, havitatudhuru.” Hivyo basi, napenda kumwambia Askofu Gwajima kwamba, Biblia hiyo inazungumzia hata nikichanja chanjo iliyokuwa na sumu kama, imani yake yeye kama Askofu, hafahamu kwamba chochote kibaya kitakachoingia kwa waumini wake hakina madhara katika miili yao sawa sawa na Biblia inavyosema. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia Biblia hiyo hiyo inasema katika Waefeso 6:12 inasema hivi, “kwa maana kwetu sisi damu na nyama, bali si juu ya wafalme na mamlaka ya nguvu za giza, vita vyetu sisi ni vya katika Ulimwengu wa Roho.” Sasa kama yeye ni mtu wa imani, kama tukibebwa katika imani kitu chochote kibaya hakitawapata Watanzania na ndivyo tulivyo na ndiyo maana tunaenda mahospitalini tunatibiwa, Wakristo wanajenga zahanati, wanajenga hospitali, kwa sababu tiba ni sehemu ya mamlaka ya Mungu. Hata Nabii Luka aliandika Kitabu cha Luka alikuwa ni daktari maana Biblia inawatambua madaktari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Biblia hiyo hiyo inasema, katika Waebrania 11:1 “imani ni kuwa na hakika na mambo yatararijiwao ni bayana na mambo yasiyoonekana.” Ukiwa na imani hakuna kitu kibaya kitakupata. Gwajima usiwakwamishe Wakristo wako na Wakristo wa Makanisa 142, imani itatulinda kama Watanzania, tutakula dawa na vitu vibaya havitatupata maana tunamwamini Mungu, na Mungu yupo katika Taifa la Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Waraka wa Tatu wa Yohana 1:2 inasema: “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yako yote, katika mambo yako ya rohoni na ya mwilini.” Hivyo basi, Biblia inatamka mwananchi wa kawaida afanikiwe mwilini, afanikiwe katika roho. Kuchoma sindano ni haki na ndiyo maana hata Gwajima akiumwa anakunywa panadol kwa kuwa Serikali inaamini Biblia inatambua katika matibabu.

Mheshimiwa Spika, walikuwepo viongozi wa dini ambao mapepo yaliwavaa; amemsema ndugu Kibwetere. Katika mwaka 2000 Machi, 17 alichoma kanisa na watu walikufa. Naomba tusimame katika imani ya Mungu, tusiwadanganye wananchi. Nanyi wananchi someni Biblia mjiamini. Ndiyo maana ukienda kujifungua, kama wewe ni Mkristo unakwenda hospitali kwa nini? Kwa sababu madaktari wana elimu ya kimungu. Hujifungulii nyumbani. Gwajima asiwadanganye watu. Ahsante. (Makofi)