Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe pongezi kwa Waziri na watendaji wake wote wa Wizara kwa kusimamia na kutekeleza majukumu yao. Wizara ya Elimu ni Wizara kubwa na hivyo ina changamoto nyingi sana ambazo Serikali na wadau wa elimu ni lazima wazitafutie majibu ya uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maboresho katika miundombinu, shule nyingi za kata zimejengwa Tanzania nzima na hivyo kupelekea watoto wengi kupata elimu, lakini shule hizi hazina maabara wala vifaa, nyumba na walimu wa madarasa ni tatizo kubwa hivyo Wizara lazima ijipange kutatua kero hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuishauri Wizara kuweka msisitizo kwa elimu ya awali (pre-school) ambako watoto wanakosa uwezo wao kiakili na kupata maarifa mapya. Kwa kuwa maandalizi ya mtaala wa elimu ya awali unaendelea ni muhimu kuangalia vigezo kwa vijana waliohitimu na kufanya vizuri katika mitihani ya kidato cha nne na sita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtaala wetu unahitaji kufanyiwa marekebisho ili uendane na dhana ya uwezo (competence based). Kwa sasa elimu yetu japo tunahubiri CBC lakini kinachoendelea mashuleni ni knowledge based. Hakuna uhalisia wa matakwa ya mtaala na kinachofanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara iwekeze katika tafiti kwenye taasisi za elimu ya juu kwa maana zimekuwa chache na taasisi hizi zimeacha moja ya jukumu lake ambalo ni ufundishaji, utafiti na ushauri wa kitaalam.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la udahili wa wanafunzi wa elimu ya juu liangaliwe upya katika sheria iliyoanzisha TCU na ikiwezekana liachwe kwa vyuo husika, na hii ndiyo practice ya vyuo vingi duniani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tujenge nchi yenye wataalam wa kada mbalimbali ni muhimu Wizara ikapiga marufuku vyuo vya kati kutoa shahada. Vyuo hivi vitoe astashahada na stashahada. Kwa sasa nchi inakosa wafanyakazi wa kawaida kwa maana wenye shahada hawawezi kufanya kazi ambazo zinaweza kufanywa na watu wa kata, ahsante.