Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naipongeza Wizara ya Elimu kwa mipango mizuri ya maendeleo. Nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Naibu Waziri na Katibu Mkuu kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuhakikisha wanafunzi wetu wanapata elimu bora. Mchango wangu nitauelekeza katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za binafsi ni nzuri sana na zinaisaidia sana Serikali kupunguzia mzigo wazazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto iliyopo ni kupanda kwa ada mara kwa mara. Ada kutozingatia hali ya uchumi wa Watanzania na kutuweka katika matabaka na kuongeza ufisadi kwa wazazi kwa kwenda kinyume na maadili ya utendaji kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu TCU, udahili wa wanafunzi wa vyuo vikuu uangaliwe upya, vyuo vya binafsi vinapelekewa wanafunzi wengi kuliko vyuo vya Serikali. Mfano UDOM ni chuo kikubwa na kina mabweni mengi lakini wanalala ndege; badala yake wanajazwa kwenye vyuo ambavyo havina hata hosteli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wa wanachuo wa private kwenda TCU ni tatizo kubwa na yawezekana ikawa sababu ya TCU kujichanganya hata kuwapa mikopo hata wasiostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali, watu wanaotaka kujilipia vyuo waende wenyewe kwenye vyuo wanavyovitaka na ada walipe kwenye chuo husika. Mfano sisi wengine ni wazee na fedha tunazo za kulipia unapelekwa TCU ukafanye nini? Usumbufu usio na msingi na kama ni kuhakiki vyeti acha nikahakikishiwe nipewe barua nimalizane na chuo husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za msingi za english medium. Shule iliyopo Dar es Salaam ni Olymipio na imezaa Diamond; ni shule zilizokuwepo kwa muda mrefu. Je, Serikali kwa nini haioneshi mpango mahsusi wa kuongeza idadi ya shule hizi angalau tukapata katika Wilaya ya Kinondoni moja na Temeke moja kwa kuanzia. Naomba Serikali iliangalie kwani Jiji la Dar es Salaam limekuwa kubwa sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matokeo ya mitihani. Kitendo cha kuwaweka wanafunzi wa shule zetu za kata na shule binafsi zenye uwiano wa mwanafunzi mmoja kwa mwalimu mmoja ni kuwaonea wanafunzi hao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunataka kushindanisha mtu ni vyema umshindanishe na yule aliyekuwepo kwenye level moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia moja bajeti ya Wizara ya Elimu changamoto zilizopo zifanyiwe kazi.