Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kuhusu ada elekezi, Serikali iwaache wamiliki kupanga bei kwa kuwa gharama za uendeshaji wa shule hizo ni kubwa sana kutokana na michango mingi na kodi. Pia shule hizi hazifanani kutoka moja hadi nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili nizungumzie kuhusu vibali vya Walimu wa nje. Serikali iangalie namna ya kuondoa vizuizi vya Walimu wa kutoka nje kufundisha Tanzania hasa Walimu wa masomo ya hesabu na sayansi. Urasimu mkubwa wa Serikali wa kupata working permit na kodi kubwa inayotozwa na Serikali inakatisha tamaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, Chuo cha VETA Geita. Naiomba Serikali kunipatia majibu ni lini chuo cha VETA kitajengwa katika Mkoa wa Geita ambao ni mpya na eneo la kujenga chuo hicho lilitengwa toka mwaka 2014. Kwa mujibu wa VETA, ujenzi wa chuo hicho ulikuwa umefadhiliwa na ADB kwa thamani ya 6.7 billion, leo miaka miwili hakuna kinachoendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nne ni kuhusu utitiri wa vyuo binafsi. Serikali ichunguze sana viwango vya elimu vinavyotolewa na vyuo mbalimbali vilivyosajiliwa na NECTA. Mfano ni Chuo cha Elimu ya Utalii Musoma kimefungua matawi katika wilaya za Kanda nzima ya Ziwa, je, ubora wa certificate na diploma hizi unafanana? Hii ni pamoja na matawi ya vyuo vikubwa na vidogo Tanzania ikiwemo CBE, Mipango na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, madeni ya wazabuni mashuleni. Serikali itoe taarifa ni lini itawalipa wazabuni fedha zao walizotumia kutoa huduma mashuleni. Hivi sasa hali ya huduma katika shule zetu ni mbaya kutokana na madeni haya ya wazabuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sita, nyumba za Walimu vijijini. Naishauri Serikali kuanzia sasa itoe tamko la kuzuia kabisa halmashauri zote kujenga nyumba za watumishi wa mjini, kuacha kujenga ofisi za vijiji na kuacha kununua magari mapya na kuhamishia pesa yote kwa miaka mitatu kwenye nyumba za Walimu. Nashauri pia ramani ya nyumba simple iandaliwe kwa ajili ya nchi nzima mfano vyumba viwili vya kulala, sitting room na jiko.