Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Makame Mashaka Foum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MASHAKA MAKAME FOUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kunijalia afya na kuweza kuchangia Wizara hii ya Elimu. Pia namshukuru Waziri na Watendaji wake wote kwa kujipanga vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali ya CCM kwa kupiga hatua kubwa kwa upande wa elimu. Anayesema Serikali haijafanya kitu, je, haoni kwa macho, hasikii, labda ana lake jambo.
Baadhi ya mafanikio kwa Serikali ya CCM ni kujenga shule za awali kutoka jumla ya shule 10,612 mwaka 2010 hadi kufikia shule 14,783 mwaka 2015 zenye Walimu 13,600. Serikali imeandikia watoto wa miaka 7-13 kutoka wanafunzi 6,499,581 mwaka 2005 hadi kufikia wanafunzi 7,679,877 mwaka 2013. Idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu imeongezeka kutoka wanafunzi 139,638 mwaka 2010
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
171
hadi kufikia wanafunzi 218,959 mwaka 2014. Mwaka huu ni mwaka wa historia, Mheshimiwa Rais baada ya kutangaza elimu bure, watoto wengi wamefurika mashuleni, haya ndiyo maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kila pawapo na mafanikio na changamoto hazikosi, la msingi ni kujipanga na kuzipatia ufumbuzi. Ufumbuzi wa changamoto kwa upande wa elimu si Wizara peke yake, hili ni jukumu letu sote jamii nzima. Mzazi analo jukumu kwa mtoto kuhakikisha anakuwa na maadili mema kuanzia nyumbani, mzazi ahakikishe mtoto anahudhuria shule na kwa wakati, mzazi ahakikishe mtoto ana afya nzuri na msafi. Serikali ihakikishe kwa kila shule vyombo vitatu viwe vinashirikiana yaani uongozi wa shule, walimu na wazazi kwa ajili ya kumpatia elimu mtoto. Wizara iweke mitaala inayoendana na mapinduzi ya viwanda na kimataifa, vitabu viwe vya aina moja kwa nchi nzima kwa madarasa yote kuepuka kila shule kusomesha mada yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara iajiri Walimu wa kutosha ili kuepuka vipindi vingi kwa mwalimu mmoja hasa katika shule za awali. Serikali ihakikishe vitabu vya kiada na ziada ni vya kutosha mashuleni. Walimu waboreshewe maslahi yao ili wafanye kazi kwa hiari. Serikali ifanye ukaguzi wa mara kwa mara kuhakikisha Walimu wanafanya kazi ipasavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia kwa mia.