Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia angalau kwa maandishi. Nitoe pongezi kwa Waziri na Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi.
Naomba kwanza kabisa kuchangia kuhusu umri wa Wahadhiri wa Vyuo Vikuu na hasa Maprofesa wanaofundisha masomo ya science; ni kweli namwomba Mheshimiwa Waziri, Serikali iongeze umri wa kustaafu kwa Wahadhiri wanaofundisha masomo au course za science mpaka miaka 70 au 75 badala ya miaka 60.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivi kwa sababu ni tabu kuwapata Walimu hawa wa science katika vyuo vikuu vyetu. Pili, Walimu hawa wanapostaafu kwa mujibu wa Sheria wakiwa na miaka 60 wanakuwa bado wanazo nguvu na afya nzuri na bado wanahitajika katika idara na hata vyuoni mwao. Kiasi wengine wengi kupitia kwenye uhitaji, chuo kinalazimika Mwalimu aendelee kufundisha kwa mkataba wa miaka miwili miwili. Naomba Mheshimiwa Waziri alione hili la kuongeza umri wa kustaafu kutoka miaka 60 mpaka miaka 70, madarasa ya awali yaangaliwe na kusimamiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, msingi wa mwanafunzi kuendelea na kupata elimu nzuri ni darasa la awali, mishahara ya Walimu hawa wa madarasa au shule za awali iangaliwe, Walimu hawa wapate mishahara yao waliyopangiwa kufuatana na daraja lao la ualimu kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mikopo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu. Urudishaji wa hela zilizokopwa na wanafunzi zirudishwe kwa wakati na mara hapo mkopaji na mhitimu wa chuo anapopata kazi, kujiajiri au kuajiriwa kwa mkakati wa wazi na mzuri wa kurudisha hela hizi, kusudi wakopeshe wanafunzi wengine kwani wahitaji ni wengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri somo la ujasiriamali litiliwe mkazo kuanzia secondari hadi vyuo vikuu ili vijana waweze kujiajiri kwenye fani mbalimbali bila matatizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.