Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Naipongeza Wizara hii kupitia Waziri, Naibu na Watendaji wote kwa kazi ngumu mnayokabiliana nayo katika Wizara hii, kwani kazi ya kusimamia na kuiendeleza taaluma kwa kiwango cha ubora ina changamoto nyingi, lakini penye nia pana njia, msivunjike moyo tuko pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimba kwa wanafunzi wa kike. Umefikia wakati sasa kwa wanafunzi wa kike wanaopata mimba baada ya kujifungua waruhusiwe kuendelea na masomo kama kuna Sheria kandamizi ziletwe Bungeni tuzibadilishe.
Bodi ya Mikopo. Pamoja na jitihada kubwa za Serikali kuwapatia mikopo baadhi ya wanafunzi wanaostahili, lakini kumekuwa na changamoto na kama Wizara/Bodi ya Mikopo haikuzifanyia uchunguzi maalum, basi ile dhana ya kuwapa mikopo wanaostahili haitafikiwa kwa usahihi na mikopo iliyoiva kushindwa kurejeshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migomo na maandamano kwa wanafunzi/wanavyuo. Kero ya maandamano na migomo kwa wanafunzi inazorotesha elimu kwani huharibu mazingira na vifaa na wakati mwingine husababisha maafa na hasara kubwa na hata shule kufungwa na wanafunzi kukosa masomo na kurudi majumbani. Wizara ina mkakati gani wa kuzuia changamoto ya maandamano na migomo, hasa kwa yale ambayo yamo ndani ya uwezo wao kwani tumeshuhudia baadhi ya wakati mara tu wanapogoma au kuandamana, kile wanafunzi wanacholalamikia Wizara inawapatia haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Dira na Dhima ya Wizara ni nzuri na kama tutaitafsiri kwa vitendo na kuwashirikisha wadau mbalimbali na kila mmoja wetu akitimiza wajibu wake hakuna lisilowezekana. Hivyo, tunaiomba Wizara iandae mipango mikakati ya muda wa kati na muda mrefu ili kubaini ushiriki mpana na wa wazi katika kufikia Dira ya Wizara ya Elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Elimu ya Juu ni suala la Muungano, hivyo pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Wizara kwa kushirikiana na upande wa Zanzibar (Wizara ya Elimu), ipo haja sasa kukaa pamoja wadau wa elimu wa pande hizi mbili za Muungano ili kubaini changamoto na kuzitafutia njia muafaka za utatuzi, hasa ukizingatia tumo katika mchakato wa ushirikiano wa Afrika Mashariki na nchi yetu pia, inakabiliwa na utandawazi. Ni muhimu tujiandae sasa, wakati hautusubiri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja hii.