Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii nami niweze kuchangia hoja hii iliyoko mbele yetu. Awali ya yote, nitamke rasmi kwamba naunga mkono hoja. Nina imani kubwa na Mheshimiwa Waziri wa Elimu. Naomba Bunge lako Tukufu, Waheshimiwa Wabunge tumuunge mkono Mheshimiwa Waziri, kwa nia yake na kwa jitihada anazozifanya kuhakikisha kwamba anarekebisha Sekta hii ya Elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri kwamba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania watakubaliana na mimi kwamba kama Taifa tuna safari ndefu kwenye Sekta hii ya Elimu.
Naweza kusema kwamba baada ya kuwa tulishapiga hatua kubwa, tulipofanya uamuzi wa kuwa na sekondari kila Kata, pamoja na kuwa na ongezeko kubwa katika Shule za Msingi, jambo hili la kuwa pia na vyuo vingi limepelekea nchi yetu kuwa katika hatua ya mpito kwenye elimu. Kwa hiyo, tutakuwa na mambo mengi ya kurekebisha mambo ambayo siyo ya siku moja, mwezi mmoja, wala miezi sita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikwambie tu, kwa kutambua hilo, ndiyo maana Mheshimiwa Rais, alitafuta mtu mahsusi, akamteua na kumleta katika sekta hii kwa kuzingatia weledi wake, na kwa kuzingatia uzoefu wake katika sekta hii. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge, tumpe muda Mheshimiwa Waziri, tumuunge mkono na Watanzania wote tumuunge mkono. Mimi naamini tunakokwenda ni kuzuri na wote tutakuja kutambua kwamba kweli Mheshimiwa Rais, alifanya jambo jema kwa kutafuta mtu mahsusi katika sekta hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukirejea kwenye historia, leo hii tunaongele kuhusu shule binafsi, shule za Serikali, ni dhahiri kwamba kinachotambulisha kwenye shule binafsi, ni dhamira ya mzazi. Kile kinachotambulisha kwenye shule ya Serikali, ni uwezo wa mwanafunzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme wazi tu kwamba Ubunge wangu niliupata kuanzia nilipofaulu kwenda sekondari. Yaani kile kitendo cha kutangazwa kwamba nimefaulu na kwenda shule ya vipaji maalum ya Ilboru, Tarafa mbili tayari zilitambua kwamba huyu ni mtu wa tofauti na tangu namaliza walikuwa wanasema ukimaliza kusoma, chagua Ubunge. Kwa hiyo, kiwango na ubora wa shule una umuhimu mkubwa sana katika kutengeneza jamii yetu na mchango wao katika maisha ya kila siku. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo, sisi kama Wabunge, ni vyema sana tukaunga mkono jitihada za Serikali; na kwakuwa ni mambo mengi ya kurekebisha, tukatoa fursa kwa Mheshimiwa Waziri na timu yake, wayafanyie kazi moja baada ya lingine. Nia ya Serikali na nia ya Mheshimiwa Rais mara zote anaposimama na anapotuelekeza, imekuwa ya dhati ya kuhakikisha kwamba heshima ya elimu inarudi kwenye mstari wake kama ambavyo amekuwa akifanya katika sekta mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niende kwenye hoja ambazo zimetolewa na Waheshimiwa Wabunge pamoja na Kamati na Taarifa ya Kambi Rasmi ya Upinzani. Kuna hoja ambayo ilitolewa kuhusu uchelewezwahji wa fedha za mikopo ya wanafunzi wa elimu wa juu, lakini taarifa zilizoko ambazo ni taarifa rasmi ni kutoka Wizara ya Fedha, zinasema, hadi Machi, 2016 kama ambavyo tunajua kwamba mikopo huwa inaenda kwa quarter, Serikali imetoa mikopo ya elimu ya juu yenye thamani ya shilingi bilioni 331.9 kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2015/2016, mikopo ya elimu ya juu Bodi ilitarajiwa kukusanya shilingi bilioni 34.7 na hadi kufikia Machi, Bodi ilikuwa imekusanya bilioni 22.9. Kwa hiyo, ukichukua na zile ambazo Serikali imetoa, utaona kwamba tayari shilingi bilioni 354 zilikuwa zimekwisha kutolewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wakati hapa na pale kunatokea ucheleweshwaji ambao ni wa kiutendaji zaidi katika masuala ya mgawanyo wa fedha, hayo ni ya kiutendaji ambayo mara zote yamekuwa yakirekebishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtakumbuka Waheshimiwa Wabunge, hali ilivyokuwa siku za nyuma na sasa iko tofauti. Zamani ilikuwa kawaida; na ilikuwa jambo la kawaida mpaka wanafunzi wagome ndiyo mikopo itoke, lakini mtakumbuka kwamba katika miaka ya hivi karibuni na siku za hivi karibuni, jambo hilo linaenda likirekebishwa, hasa hasa yamekuwa tu yakitokea yale ambayo ni ya kiutendaji ya ndani ya usambazaji wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo lilijitokeza lilikuwa ni fedha za mchango wa Serikali, Mradi wa Mlonganzila, ambao kwa bajeti ilikuwa inatarajiwa zitumike dola milioni 755. Tayari Serikali ilishachangia shilingi bilioni 18 na tayari zilishalipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo Waheshimiwa Wabunge wamelisema, ni lile ambalo linahusu pendekezo la bajeti ya Wizara ya Elimu pamoja na TAMISEMI angalau kuongezeka kutoka asilimia 11 kwenda 15 hadi 20. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba kwa hesabu zetu tulizozipiga; na hii ni taarifa rasmi kutoka Wizara ya Fedha, kwamba tayari tumeshavuka hiyo asilimia inayopendekezwa na Waheshimiwa Wabunge na sasa tuko asilimia 22 ambayo ni shilingi bilioni 4,777 za bajeti yote. Kwa hiyo, tayari Serikali imeshavuka lengo hilo ambalo Waheshimiwa Wabunge wanapendekeza la kufika asilimia 20, sasa tuko asilimia 22.1. (Makofi)
Jambo lingine ambalo liliongelewa ni kuhusu madai ya Walimu yasiyo ya mishahara. Serikali imechukua hatua, tayari imetenga fedha zaidi ya shilingi bilioni 626 kwa ajili ya kushughulikia madeni ambayo yamehakikiwa. Kingine kikubwa ambacho Serikali imefanya ni kuhangaika na mianya iliyokuwa inasababisha malimbikizo ya aina hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utaratibu uliopita, ilikuwa inatokea Waalimu wakitaka kufanyiwa promotion, kubandishwa madaraja, walikuwa wanaulizwa. Kwa hiyo, ilikuwa inatokea Mwalimu ambaye amesoma Chuo kimoja na mwenzake, wamepangiwa vituo kwa wakati mmoja; lakini ikitokea yeye akachelewa kupokea barua ambayo inaelezea kuhusu kupandishwa kwake, ilikuwa inatokea Waalimu waliosoma pamoja, wamepangiwa kazi pamoja, wanapandishwa madaraja tofauti kufuatana na kupokea taarifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali itaenda moja kwa moja kuwapandisha watu ambao wana sifa bila kuwauliza kwa sababu ni dhahiri kwamba hakuna mtu atakataa kupandishwa daraja kama amefuzu sifa zile ambazo zinatakiwa, atapandishwa. Hiyo itaondoa Walimu ambao wamemaliza pamoja na wamepangiwa pamoja kazini, wameanza kazi pamoja kuwa na madaraja tofauti kama walivyopandishwa.