Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia. Kwanza kabisa namshukuru Waziri kwa hotuba yake nzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nianze kuchangia mchango wangu. Mkoa wetu wa Simiyu ni wakulima wazuri wa pamba lakini cha kusikitisha zao hilo linaenda kufa kabisa, wananchi wamekata tamaa kabisa kwa sababu ya bei kushuka. Suluhisho pekee la bei ya pamba ni kutuletea kiwanda cha nguo na nyuzi. Mkituletea kiwanda cha nyuzi, nina imani vijana wengi watapata ajira na bei ya pamba itapanda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wetu wa Simiyu tuna viwanda vitano vya kuchakata pamba. Naona na wenye ginneries wamekata tamaa, nashindwa kuelewa kwamba zao la pamba likifa viwanda vile vitafanya kazi gani. Naomba mtuletee kiwanda cha nyuzi na kiwanda cha nguo, nina imani hata wao watauza marobota yao karibu zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia mkoa wetu ni wa wafugaji, tunaomba mtuletee kiwanda cha nyama. Nasema hivyo kwa sababu wafugaji wetu wanaibiwa sana, wakipeleka mnadani ng‟ombe mmoja anauzwa shilingi laki mbili mpaka shilingi laki tatu lakini ng‟ombe huyo huyo ukimlisha na kumnenepesha ukimpeleka kiwandani unamuuza shilingi laki nane mpaka shilingi milioni moja, naomba mtuletee kiwanda cha nyama. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Simiyu kuna akinamama wajasiriamali wakubwa na wazuri sana, wana vikundi vikubwa. Naomba Serikali iwaletee viwanda vidogo vidogo vya SIDO vya kusindika mazao ili waweze kujikwamua na umaskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, ya kwangu yalikuwa ni machache tu ya kuomba viwanda, Serikali yangu ni sikivu, naomba ituletee viwanda hivyo katika Mkoa wetu wa Simiyu. Ahsante sana.