Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba na mimi nichangie katika Wizara hii ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.
Katika nchi yetu tuna rasilimali za kutosha ikiwa ni pamoja na madini, mazao, bandari, mbuga za wanyama, mifugo. Mkoa wa Njombe ni moja ya mikoa mitano inayozalisha mazao ya chakula na mazao ya biashara. Mazao ya chakula ni kama matunda, viazi, mahindi, ngano, maharage na kadhalika; mazao ya biashara ni pamoja na chai, mbao na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hadi sasa Mkoa wa Njombe hauna viwanda vinavyoeleweka. Naomba Serikali ione ni namna gani inapeleka wawekezaji watakaosaidia kuanzisha viwanda vya kripsi zinazotokana na viazi, viwanda vya mbao; viwanda vya karatasi, viwanda vya mafuta ya alizeti na viwanda vya juice.
Pia Serikali iwasaidie wajasiriamali wadogo wadogo ili kuanzisha viwanda vidogo vidogo kama vile viwanda vya vikapu, mapambo, sabuni na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha, ahsante.