Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, maendeleo ya uhakika yatakayotupeleka kwenye nchi ya uchumi wa kati yatapatikana kwa kuwa na viwanda, tena viwanda vinavyotumia mazao yetu kama malighafi yake. Kufikia uchumi wa kati ni kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja ambao kwa ujumla wake ndio utakaopandisha uchumi wa nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza na kuunga mkono hoja ya Wizara kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijielekeza Mkoani kwangu Dodoma, Wilayani kwangu Chamwino na Jimboni kwangu Chilonwa, naomba kuomba yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iweke mazingira rahisi kwa wananchi wa Jimbo la Chilonwa kuweza kukipa na kuanzisha viwanda vidogo vidogo vinavyochakata/process mazao yanayozalishwa jimboni kama vile mashine za kukamua alizeti, ufuta pia, mashine za ku-process mahindi na kuuza sembe mijini badala ya kuyauza mahindi (value addition).
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kipekee zao la zabibu ambalo kwa hakika ndio mkombozi wa uchumi wa wananchi wa Dodoma ambao bado unasinzia. Kwa zabibu naiomba Wizara ifanye kufuatilia Halmashauri ya Chamwino ili kuisaidia kufanikisha ujenzi wa kiwanda cha zabibu cha kisasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda cha kisasa ni kile kitakachowezesha uzalishaji wa juice, mvinyo na concentrate ya mvinyo. Hiki ni kiwanda tofauti na vile vidogo vidogo na vichache vilivyopo vinavyozalisha mvinyo tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.