Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sera ya kuwekeza kwenye viwanda, nashauri tujikite zaidi kwenye viwanda vidogo vidogo vyenye kuongeza thamani ya mazao yetu badala ya viwanda vya kuzalisha bidhaa kamili kama hatuna “comparative advantage” ya bidhaa za aina hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali itafute mwekezaji wa Kiwanda cha kusindika samaki katika Kisiwa cha Mafia sambamba na kupata meli za uvuvi zenye zana za kisasa zenye uwezo wa kuvua katika bahari ya kina kirefu. Mafia ipo karibu na mkondo wenye kina kirefu kunapopatikana samaki wengi na wakubwa wa aina mbalimbali kama Jodari (Tuna) nguva (King fish) samsuri (Marley) na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uzalishaji wa viwanda vya sukari umekuwa mdogo na hautoshelezi kulisha soko la nchi nzima. Ipo hoja na haja ya kuvutia mwekezaji kuwekeza katika bonde la Mto Rufiji ili kuondokana na tatizo la kuagiza sukari kila mwaka. Naishauri Serikali pia katika kipindi hiki kuelekea kujitosheleza kama uzalishaji wa ndani wa sukari, Serikali itoe vibali kwa kuagiza sukari kwa viwanda vyenyewe, mfano, Mtibwa, Kagera na kahalika.