Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara iwasaidie wakulima wa mazao ya baharini:-
(i) Kuwatafutia masoko ya uhakika wakulima wa zao la mwani;
(ii) Kusaidia kuwapatia elimu juu ya mbegu bora ya mwani inayokubalika katika masoko ya nje ya nchi; na
(iii) Kuhamasisha wawekezaji wawekeze katika kujenga viwanda vya usindikaji wa mazao ya bahari, mfano mwani na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara iongeze juhudi katika kudhibiti uingizaji wa bidhaa zisizo na ubora unaokubalika kwa matumizi na zinazohatarisha maisha ya mtumiaji na hasa bidhaa za chakula.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uanzishaji wa viwanda uzingatie ujenzi wa viwanda visivyoharibu mazingira, malighafi zake ziwe zinapatikana hapa nchini, Wizara iweke vipaumbele vya aina ya viwanda tutakavyoanza navyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho napongeza juhudi za Wizara katika juhudi zake za kufufua viwanda na kuanzisha vipya kwa nia ya kuongeza pato la Taifa na kupunguza tatizo la ajira kwa wananchi na kuweza kunyanyua hali zao za maisha. Ahsante.