Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa pongezi kwa namna unavyoliongoza Bunge. Naomba kuchangia Wizara ya Viwanda na Biashara kwa maandishi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Kigoma Kusini liko Wilaya ya Uvinza, Mkoa wa Kigoma na ni Jimbo ambalo wananchi wake wanajishughulisha na kilimo cha michikichi pia ni wavuvi. Naomba Waziri aone namna ya kuwapatia wananchi wa uvinza miche ya michikichi ya kisasa inayozaa kwa muda mfupi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema haya kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amesema wawekezaji wako tayari kuja kuanzisha viwanda vya mawese Uvinza. Namwahidi Mheshimiwa Waziri kama Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini, niko tayari kuhamasisha wakulima wa zao la michikichi, kulima zao hili kwa nguvu zote na mimi pia nitakuwa mfano wa kulima zao hili la michikichi. Hivyo, namwomba Mheshimiwa Waziri atupe kipaumbele kutuletea mbegu ya michikichi ya muda mfupi ili na sisi wananchi wa Uvinza tuweze kupata wawekezaji wa kuja kuanzisha viwanda. Pia nampongeza sana Waziri kwa mipango yake mizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie viwanda vya uvuvi. Wananchi wa Uvinza pia ni wavuvi wa samaki na dagaa, hivyo, kwa kuwaanzishia viwanda itawasaidia wavuvi kupandisha thamani mazao haya ya uvuvi. Hivyo naomba Mheshimiwa Waziri, mipango yako hii mizuri izingatie kuwaletea wananchi wa Jimbo la Kigoma Kusini viwanda vya Mawese na Viwanda vya Uvuvi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.