Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya Wizara ya Ardhi mwaka 2011/2012 Bunge lilipitisha matumizi ya kuanzisha mabaraza ya ardhi na nyumba Wilaya ya Matano na Tunduru ikiwa ni mojawapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, Baraza la Ardhi la Nyumba halikuanzishwa na Serikali kutokana na bajeti ya Wizara kwa muda uliopangwa. Ndipo Halmashauri kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ikafuatilia Serikalini mipango hiyo ya uanzishwaji wa Baraza. Jibu lililotolewa ni kwamba Serikali kwa sasa haina uwezo wa kuanzisha Baraza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia kwamba wananchi wa Tunduru wanapata taabu ya kusafiri kilometa 264 hadi Songea kufuata huduma za baraza. Halmashauri ikaona ni vema itoe jengo miongoni mwa majengo ya Idara ya Ujenzi na samani japo chache ili angalau Baraza liweze kufanya kazi. Je, ni lini Serikal itaajiri Mwenyekiti wa baraza la Ardhi la Wilaya ya Tunduru? Kwa
sasa Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi la Songea Mheshimiwa Norbet Ndimbo ndiye anaetembelea Baraza la Tunduru kila baada ya mwezi mmoja na mara nyingine miezi miwili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itaajiri watumishi na wahudumu wa Baraza? Kwa sababu sasa kuna mtumishi mmoja Bi. Vumilia Chipasura anafanya kazi ya Uhudumu, Ukarani na Uchapaji. Ikiwezekana basi, hata huyo kibarua aangaliwe kama ana sifa aajiriwe na aongezewe watumishi wengine kwani amejitolea kwa muda wa miaka miwili sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri Serikali ijenge jengo la kudumu kwa ajili ya Baraza la Ardhi badala ya kuazima jengo Halmashauri. Hii iendane na ununuzi wa thamani za Ofisi.