Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda kumpongeze Mheshimiwa Waziri kwa jitihada zake za kuhamasisha viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada hizo, Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni kuwa kutajengwa kiwanda cha samaki na utengenezaji wa boti: Je, mpango huo ukoje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliwahi kufuatilia TBS kwa ajili ya kujenga shades za kukaushia samaki na dagaa, ikiwa ni sehemu ya kusaidia MSMES na SMEs. Napenda kufahamu je, Wizara ina fahamu juu ya hilo ili kuendelea kuwasukuma TBS ikiwa ni sehemu ya mafunzo katika suala la usindikaji wa dagaa na samaki wenye ubora?
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hao wamekuwa waki-process dagaa katika mazingira duni, mbaya zaidi kuondoa sura nzuri ya fukwe za Ziwa Nyasa. Angalau basi tusaidiwe eneo la Mbamba Bay.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini Mheshimiwa Waziri atasaidia kwa kuagiza taasisi zake TBS, SIDO na wengine anaowajua ili kusaidia na kuleta tofauti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri, asaidie kabla wananchi hawajanitumbua.