Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kidogo katika hoja hii muhimu katika kujenga Taifa letu. Ili nchi iendelee ni lazima iwe na viwanda vinavyozalisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natoka Mkoa wa Kilimanjaro ambao ulikuwa na viwanda kadhaa ambavyo vilichangia pato la Taifa, lakini kwa bahati mbaya hakuna kiwanda kinachofanya kazi kwa sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nisemee Kiwanda cha Magunia Moshi. Kiwanda hiki kimeshindwa kwa sababu kumekuwa na uingizaji mkubwa wa magunia toka nje na bei ya magunia hayo iko chini kuliko haya magunia yanayotengenezwa nchini kwetu na sababu kubwa ni kodi nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni kwanini nchi yetu kupitia Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki hamkai na kukubaliana kuzuia uingizaji wa magunia toka nje ili viwanda vilivyo ndani ya nchi zetu hizi viweze kufanya kazi na kuzalisha na kutoa ajira kwa wananchi wa nchi hizi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, kuna umuhimu wa Serikali kukaa na wawezeshaji ili kujua matatizo waliyonayo ili kuondoa matatizo hayo waweze kuzalisha na hata kuuza bidhaa zao wanazozalisha toka kwenye viwanda vyao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, namwomba Mheshimiwa Waziri atusaidie Mkoa wetu wa Kilimanjaro, tuna tatizo la ardhi. Je, Wizara ina mpango gani wa kututafutia wawekezaji wa viwanda vidogo vidogo kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa wetu pamoja na Wabunge tunaotoka kwenye Mkoa huo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hayo ndiyo niliyotaka kuchangia kuhusu Mkoa wangu. Nategemea Mheshimiwa Waziri na wataalam wake wanafanyia kazi mambo hayo ili Mkoa wetu uweze kurudi kwenye hali yake ya zamani ya kiuchumi na kutoa ajira kwa wananchi wa Mkoa wetu.